HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, May 16, 2025

NBAA NA ZIAAT ZASAINI MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO WA MIAKA MINNE

    

Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  Tanzania (NBAA) na Taasisi ya Wahasibu,  Wakaguzi na Washauri elekezi wa Kodi Zanzibar (ZIAAT) zimesaini hati ya makubaliano ya kufanya kazi pamoja katika maeneo mbalimbali yanayohusu taaluma ya uhasibu na ukaguzi wa hesabu. Makubaliano haya ya miaka minne, yanayoweza kuongezwa muda baada ya kumalizika, yana lengo la kuimarisha ukuaji na uendelevu wa taaluma hii nchini.

Makubaliano hayo yanarahisisha ushirikiano kati ya NBAA, ambayo hapo awali ilikuwa ikifanya kazi Tanzania Bara, na ZIAAT, inayoshughulikia Zanzibar. Kupitia ushirikiano huu, NBAA sasa itaweza kufanya kazi Zanzibar kwa kushirikiana na ZIAAT, na vivyo hivyo ZIAAT itaweza kufanya kazi Tanzania Bara kwa ushirikiano na NBAA.

Miongoni mwa maeneo ya ushirikiano ni uandaaji na uendeshaji wa mafunzo endelevu, Masuala ya uanachama, Masuala ya mitihani na Masuala ya ufundi.

Hatua hii ni muhimu kwa kuimarisha taaluma ya uhasibu nchini, ikiwa ni pamoja na kurahisisha utendaji kazi wa taasisi hizi mbili katika Tanzania Bara na Visiwani, na hivyo kuleta maendeleo ya pamoja katika sekta hii.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  Tanzania (NBAA) CPA Pius Maneno (kulia)  pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Wahasibu,  Wakaguzi na Washauri elekezi wa Kodi Zanzibar (ZIAAT) CPA Ame B. Shadhil(kushoto) wakionesha hati ya makubaliano ya kufanya kazi pamoja katika maeneo mbalimbali yanayohusu taaluma ya uhasibu na ukaguzi wa hesabu mara baada ya kuingia makubaliano ya miaka minne. 
Mgeni rasmi Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Dkt. Juma Malik Akil  akishuhudia utiaji saini kati ya NBAA na ZIAAT  uliofanywa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  Tanzania (NBAA) CPA Pius Maneno na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Wahasibu,  Wakaguzi na Washauri elekezi wa Kodi Zanzibar (ZIAAT) CPA Ame B. Shadhil
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  Tanzania (NBAA) CPA Pius Maneno (kulia) wakipongezana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Wahasibu,  Wakaguzi na Washauri elekezi wa Kodi Zanzibar (ZIAAT) CPA Ame B. Shadhil(kushoto)mara baada ya saini hati ya makubaliano ya kufanya kazi pamoja katika maeneo mbalimbali yanayohusu taaluma ya uhasibu na ukaguzi wa hesabu. 
Picha za pamoja


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad