Muyenzi alisema tayari
kiasi cha Shilingi Bilioni 7.2 ya mapato hayo ya ndani kimeshaelekezwa kwenye
shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo miradi ya elimu, afya, kilimo,
miundombinu na biashara.
Amesema mbali na
mapato ya ndani kwa mwaka huu wa fedha pia Manispaa ya Geita imepokea kiasi cha
Shilingi Bilioni 2.63 kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya kuboresha huduma za
kijamii.
Ameeleza pia wamepokea
Shilingi Milioni 204 kati ya Shilingi Milioni 422 kutoka Mgodi wa Uchimbaji wa
Madini ya Dhahabu wa Geita (GGML) Pesa za uwajibikaji wa kampuni kwa jamii
(CSR) kutekeleza miradi viporo ya mwaka 2018-2021.
Meya wa Manispaa ya
Geita, Costantine Morandi amesema makadirio ya mapato ya ndani yamepanda kwa Shilingi
Bilioni 11 ndani ya miaka mitano kutoka Shilingi Bilioni 5 mwaka 2020 hadi Shilingi
Bilioni 19 mwaka 2025.
Katibu wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) wilaya ya Geita, Michael Msuya amepongeza halmashauri kwa niaba
ya chama na kukiri wazi kuwa viongozi waliopewa dhamana ndani ya manispaa
wanawajibika.
No comments:
Post a Comment