TEA ilikuwa miongoni mwa taasisi zaidi ya 30 zilizoshiriki katika maonyesho hayo yaliyoandaliwa na Mfuko wa Utamaduni, kwa lengo la kuhamasisha na kuendeleza shughuli za kitamaduni nchini.
Vigezo vilivyotumika katika kutoa tuzo hizo ni pamoja na muonekano wa banda, utoaji wa huduma kwa wageni waliotembelea banda, pamoja na muda wa kufungua na kufunga huduma.
Tuzo hizo zilitolewa na Mgeni Rasmi, Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mhe. Prof. Paramaganda Kabudi, ambaye alipongeza taasisi zote zilizoshiriki kwa mchango wao katika kufanikisha maonyesho hayo.








No comments:
Post a Comment