Umuhimu wa kutoa taarifa kwa wakati kwa waliofanyiwa ukatili wa kijinsia unasaidia kuzingatia afya na kupata matibabu mapema maana wananchi wengi wamekuwa na tabia wanachelewa kutoa taarifa na kuhatarisha afya zao.
Kaimu Mwenyekiti (TPF-NET) Mkoa wa Geita, Kaijage amesema hayo kwa Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Geita iliyopo Mjini Geita kabla ya kukabidhi misaada mbalimbali kwa wanafunzi hao.
Katibu Tawala wa Wilaya ya GEITA Lucy Beda amepongeza hatua ya Mtandao wa Polisi Wanawake wa Mkoa wa GEITA kufika katika shule ya sekondari na kutoa elimu na wajitahidi kufika hadi vijijini maana wengine wanaona kitendo cha ukatili ni matendo ya kawaida.
No comments:
Post a Comment