Mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa CCM pamoja na viongozi wa serikali, akiwemo wakuu wa idara wa Manispaa ya Shinyanga.
Mongella ameanza ziara ya siku saba mkoani Shinyanga kwa lengo la kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020-2024 na kuimarisha uhai wa chama. Katika ziara hiyo, atafanya mikutano ya hadhara na ya ndani ili kusikiliza changamoto zinazowakabili wananchi wa mkoa wa Shinyanga.
Ziara hiyo itamfikisha katika maeneo ya Shinyanga Vijijini, Kahama, Msalala, Kishapu, na Ushetu, ambako atakutana na viongozi wa chama na wananchi kujadili namna bora ya kuimarisha utekelezaji wa sera za chama kwa maendeleo ya mkoa.
Pia, ziara hii inalenga kuwahamasisha wanachama wa CCM kushiriki kikamilifu katika shughuli za chama na kushughulikia kero za wananchi.











No comments:
Post a Comment