HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, May 18, 2024

WAZIRI MKUU MGENI RASMI KONGAMANO LA WAANDISHI WA HABARI WA VYOMBO VYA MITANDAO YA KIJAMII

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Jumuiya ya Mitandao ya Kijamii Tanzania (JUMIKITA) kwa kushirikiana na Shirikisho la Serikali za Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Tanzania (TAHLISO) wameandaa kongamano la waandishi wa habari wa vyombo vya mitandao ya kijamii nchini kwa lengo la kuimarisha wigo wa utoaji wa habari kupitia mitandao ya kijamii na mipango mbalimbali ya maendeleo.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kongamano hilo linalotarajiwa kufanyika Jumatatu Mei 20, 2024 katika ukumbi wa maktaba katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 18, 2024 Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa JUMIKITA Shaaban Matwebe amesema Kongamano hilo linatarajiwa kuwa na washiriki zaidi ya 500, ambapo mada mbalimbali zitajadiliwa ikiwa ni pamoja na mitandao ya kijamii na uzalendo, fursa zilizopo kwenye tasnia hiyo, mafanikio na changamoto ili kutoa mchango wa kiundeshaji kwa wadau kupitia JUMIKITA.

"Tutatoa pia mapendekezo yatakayosaidia serikali kwenye uratibu wa sera za jinsi ya kuunganisha sayansi ya uchumi wa taarifa (information economics) na uchumi wa taarifa (information economy)". Amesema

Aidha amesema kuwa Kongamano hilo litajadili mafanikio ya miaka mitatu ya serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ikiwa ni pamoja na maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari duniani.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mitandao ya Kijamii Tanzania (JUMIKITA), Shaaban Matwebe akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa ya ujio wa Kongamano la Waandishi wa Habari wa mitandao ya Kijamii litakalofanyika Mei 20,2024 katika ukumbi wa Maktaba Mpya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Kassim Majaliwa.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mitandao ya Kijamii Tanzania (JUMIKITA), Shaaban Matwebe akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa ya ujio wa Kongamano la Waandishi wa Habari wa mitandao ya Kijamii litakalofanyika Mei 20,2024 katika ukumbi wa Maktaba Mpya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Kassim Majaliwa.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mitandao ya Kijamii Tanzania (JUMIKITA), Shaaban Matwebe akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa ya ujio wa Kongamano la Waandishi wa Habari wa mitandao ya Kijamii litakalofanyika Mei 20,2024 katika ukumbi wa Maktaba Mpya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Kassim Majaliwa.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad