Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amewataka wakandarasi wazawa waliopewa dhamana ya ujenzi wa Miradi ya umwagiliji kuhakikisha waaitekelza kwa weledi na ubora wa hali ya Kuu.
Majaliwa
Ameyasema hayo Jana katika hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa
Miradi ya umwagiliaji katika maeneo mbalimbali, iliyofanyika jijini
Dodoma.
"Ndugu washiriki nimefurahishwa kuona kuwa asilimia 82 ya
wanaokwenda kujenga miradi hii ni wataalamu na hizi ni fursa za ajira
kwa Watanzania, lakini ni fursa ya kuongeza ujuzi kupitia miradi hii,
vilevile inakwenda kuongeza kipato kwa Watanzania.
"Nitoke rai
kwa wakandarasi wazawa, kwanza mbadilike, mnathaani kubwa mmepewa ya
kutekeleza miradi na hili ndicho kilio kikubwa cha private seckta (sekta
binafsi) leo mmeona serikali imeendelea kutekeleza kwa kuwapa miradi.
"Mjipange
vizuri tumieni fursa hii kuihakikishia serikali kwamba mnaweza, lakini
nyie mna dhamira zenu kufungua kampuni za ukenzi, mna hiyo dhamira
simamieni dhamira zenu. Sisi tunakutegemeeni nyie kufua milango ya
ajira.
No comments:
Post a Comment