HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, May 5, 2024

MRADI WA KUENDELEZA LISHE NA UFUGAJI ENDELEVU WA VIUMBE MAJI KWA WAKULIMA WADOGO YAZINDULIWA MPITIMBI

Na; Mwandishi Wetu – Songea

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya (Sera, Bunge na Uratibu), Mhe Jenista Mhagama amezindua Mradi wa kuendeleza lishe na ufugaji endelevu wa viumbe maji kwa wakulima wadogo (ARNSA) katika kijiji cha Mpitimbi kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea Vijijini Mkoani Ruvuma Tarehe 4 Mei 2024.

Mradi huo wa kuendeleza lishe na ufugaji endelevu wa viumbe maji kwa wakulima wadogo (ARNSA) unaoenda kutekelezwa katika Wilaya nne za Mikoa ya Ruvuma na Lindi, na kulenga katika kunufaisha kaya elfu Moja (1000) katika Wilaya za Songea vijijini, Mbinga Mkoani Ruvuma, Ruhangwa na Mtama Mkoani Lindi, ambapo pamoja na mambo mengine Familia na jamii hizo zinaenda kuinua hali ya maisha kwa kuongeza kipato na kuimalisha Lishe.

Akiongea katika uzinduzi wa mradi huo,Waziri Mhagama alisema Mpitimbi imebahatika kuanza na mradi huu, na kwakuwa Mkoa wa Ruvuma unaongoza kwa uzalishaji wa mazao ya chakula lakini, una changamoto ya udumavu,”Na ndiyo maana Serikali imeleta mradi huu ambao utatumia takribani zaidi ya shilingi Bilioni tatu nukta moja, katika maeneo tuliyojipangia, ambao ni sehemu ndogo tuu ya Programu kubwa ya kuendeleza sekta ya Kilimo na Uvuvi, Tumebahatika kuanza na mradi huu unaofadhiliwa na ubalozi wa Norway Nchini hivyo ni wakati mzuri wa Wilaya zitakazonufaika kuweza kujikimu kimapato na kiafya.” Alisema.

Aliendelea kusema kuwa, kwa kuwa hali ya udumavu inaleta changamoto ya afya ya akili ni fursa sasa kwa wananchi wa mkoa wa Ruvuma kuendelea kuboresha afya, kupitia lishe ya viumbe maji na hasa Samaki.

Waziri Mhagama aliushukuru ubalozi wa Norway kupitia shirika lake la NORAD kuleta mradi huo mkoani Ruvuma, “Leo Tunazindua Shamba Darasa Ambalo linaenda kuchagiza maendeleo ya tabianzuri ya biashara na matumizi ya lishebora kupitia samaki wanaofugwa kwenye mabwawa, na miradi itakayofanywa kwenye baadhi ya halmashauri za Mkoa wa Ruvuma.” Alisisitiza.

Alibainisha kuwa, Kupitia bwawa kubwa la Asili lililopo Mpitimbi ni wakati sahihi sasa wa kuimarishwa kwa bwawa hilo na kuanza kwa ufugaji mkubwa wa Samaki “Tunatamani kuona kuwa Bwawa hilo lenye ukubwa wa hekari 17.4 linaendelezwa na kuwa shamba Darasa.” Alisema

Awali, Waziri Mhagama Alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa, kupeleka Miradi mingi ya Maendeleo katika Mkoa wa Ruvuma.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Bw. Anderson Mutatembwa alisema, kupitia mradi huo unaoenda kutekelezwa kwa miaka miwili,Tanzania imekuwa Miongoni mwa nchi tatu za Afrika kupata bahati ya kunufaika na Mradi huo, zikiwemo nchi za Kenya na Msumbiji.

Aliendelea kusema kuwa, mradi huo wa kuendeleza Lishe na ufugaji endelevu wa viumbemaji na ukulima wa mwani kwa wakulima wadogo unatekelezwa katika mikoa kumi na moja ya Tanzani Bara pamoja visiwa vya unguja na Pemba.

Akiongea katika ghafla hiyo muwakilishi kutoka Mfuko wa Kimataifa wa maendeleo ya Kilimo nchini (IFAD) Bi. JacquiIine Machangu Motcho aamesema, IFAD imekuwa ikifanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika nyanja na sekta zinazolenga, kutatua changamoto mbalimbali zinazoikumba sekta ya kilimo hususani Wakulima wadogo wadogo hasa wale walio vijijini.

Na aliendelea kusema kuwa, Shirika hilo limeendelea pia kuyapa kipaumbele maeneo hayo ikiwa na dhamira ya kuinua na kuboresha sekta ya Kilimo, Mazao, Mifugo na Uvuvi ili kufikia uzalishaji wa juu ulio endelevu na wenye faida kibishara, unaoleta ukuaji wa pamoja kiuchumi na Taifa zima kwa ujumla.

Akizungumza kuhusu mradi huo, Bi JacquiIine alisema Kupitia Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi, IFAD imepokea ufadhili-ruzuku(grant) kwa mradi wa ARNSA kutoka Ubalozi wa Norway, unaolenga kupunguza umaskini na kuboresha lishe kupitia shughuli za Ufugaji wa Samaki wenye tija na ustahimilivu kutoka kwa wazalishaji/wafugaji wadogo. Dhamira yake ya kimaendeleo inalenga kuongeza mapato, kujenga ustahimilivu na kuwajengea uwezo kimaisha wafugaji wadogo wa samaki walio vijijini.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama akizungumza katika Uzinduzi wa mradi wa kuendeleza lishe na ufugaji endelevu wa viumbe maji kwa wakulima wadogo (ARNSA), uliyopo chini ya Progamua ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP), katika kijiji cha Mpitimbi Wilayani Songea Vijijini Tarehe 4 Mei, 2024
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Bw. Anderson Mutatembwa, akitoa Neno la Utangulizi wakati wa Uzinduzi wa mradi wa kuendeleza lishe na ufugaji endelevu wa viumbe maji kwa wakulima wadogo (ARNSA), uliyopo chini ya Progamua ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP), katika kijiji cha Mpitimbi Wilayani Songea Vijijini Tarehe 4 Mei, 2024

Picha ikionesha Baadhi ya washiriki wakati wa Uzinduzi wa mradi wa kuendeleza lishe na ufugaji endelevu wa viumbe maji kwa wakulima wadogo (ARNSA), uliyopo chini ya Progamua ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP), katika kijiji cha Mpitimbi Wilayani Songea Vijijini Tarehe 4 Mei, 2024
Muwakilishi kutoka Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo nchini (IFAD) Bi. JacquiIine Machangu Motcho, akizungumza wakati wa Uzinduzi wa mradi wa kuendeleza lishe na ufugaji endelevu wa viumbe maji kwa wakulima wadogo (ARNSA), uliyopo chini ya Progamua ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP), katika kijiji cha Mpitimbi Wilayani Songea Vijijini Tarehe 4 Mei, 2024
Aliyeinama, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama, akiweka mbegu ya Samaki katika moja ya Bwawa, wakati wa Uzinduzi wa mradi wa kuendeleza lishe na ufugaji endelevu wa viumbe maji kwa wakulima wadogo (ARNSA), uliyopo chini ya Progamua ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP), katika kijiji cha Mpitimbi Wilayani Songea Vijijini Tarehe 4 Mei, 2024


Picha ya pamoja Baadhi ya washiriki, baada ya Uzinduzi wa mradi wa kuendeleza lishe na ufugaji endelevu wa viumbe maji kwa wakulima wadogo (ARNSA), uliyopo chini ya Progamua ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP), katika kijiji cha Mpitimbi Wilayani Songea Vijijini Tarehe 4 Mei, 2024

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad