HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, May 6, 2024

BARRICK YADHAMINI KONGAMANO LA WANAFUNZI VYUO VIKUU VYA IRINGA NA DODOMA

 

Mratibu wa mafunzo (Supervisor Learning and Development wa Barrick Tanzania,Elly shimbi akiongea na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma wakati wa kongamano lakuwajengea uwezo wakujiamini na kuhimili ushindani wa ajira na kujiajiri lililoandaliwa na taasisi ya AIESEC Tanzania lililofanyika katika chuo hicho mwishoni mwa wiki kwaudhamini wa Barrick.
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma na vyuo vya elimu ya juu mkoani humo wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa kongamano hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa ,Mayeka Simon Mayeka akiongea katika kongamano hilo.
Na Mwandishi Wetu.

Kampuni ya madini ya Barrick nchini, imedhamini na kushiriki katika kongamano la wanafunzi wa vyuo vikuu vya Dodoma na Iringa lililoandaliwa na taasisi ya kuchipua na kuendeleza vipaji vya uongozi kwa vijana (AIESEC Tanzania) lililofanyika katika vyuo hivyo na kuwashirikisha wanafunzi wanaosoma vyuo vya elimu ya juu,wahadhiri na wadau mbalimbali.

Kupitia makongamano haya ambayo hufanyika kila mwaka, wanafunzi huweza kufahamu jinsi taasisi mbalimbali nchini zinavyoendesha shughuli zake lengo kubwa ikiwa ni kuwajengea uwezo wa kujua vipaji walivyonavyo, kujifunza jinsi ya kujiamini na kukabiliana na ushindani katika soko la ajira,kujiamini kwa kujiajiri,kuchangamkia fursa zinazojitokeza na kujitambua uwezo wao ni jinsi gani wanaweza kushiriki kutoa mchango wa kuendeleza taifa pindi wamalizapo masomo yao.

Maofisa Raslimali Watu Waandamizi na wataalamu mbalimbali kutoka Barrick pia walishiriki katika maonesho na kongamano hayo ambapo walipata fursa kuzungumza na wanafunzi kuhusiana na kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo ajira,kuendeleza vipaji vyao pia wanafunzi walipata fursa kuelewa jinsi kampuni ya kimataifa ya dhahabu ya Barrick, inavyoendesha shuguli zake kwa kutoa kipaumbele kusaidia jamii sambamba na mpango wake wa kuibua na ukuzaji wa vipaji kwa vijana wa kitanzania,kuwezesha wanawake kuingia katika sekta na wafanyakazi wake.

Wanafunzi kutoka vyuo hivyo walipata fursa ya kuuliza maswali mbalimbali kuhusiana na ajira kwa wataalamu wa fani ya Raslimali kutoka makampuni mbalimbali walioshiriki katika makongamano hayo.

Akiongea katika kongamano lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma, Mkuu wa Wilaya ya Kongwa ,Mayeka Simon Mayeka ambaye alikuwa mgeni rasmi aliwataka wanafunzi kujiamini wakati wote na kuchangamkia fursa mbalimbali zinazojitokeza zikiwemo za ajira na kujiajiri.
Alisema zama hizi na maisha ya kidigitali vijana wanayo nafasi kubwa kupata mafanikio iwapo wataandaliwa vizuri.Alipongeza taasisi ya AIESEC Tanzania kuandaa makongamano ya kuwajengea uwezo wanafunzi vyuoni pia aliipongezakampuni ya Barrick kwa kudhamini makongamano haya.
Wataalamu kutoka Barrick wakiongea katika kongamano la wanafunzi wa Chuo kikuu cha Iringa lililoandaliwa na na taasisi ya AIESEC Tanzania lililofanyika katika chuo hicho mwishoni mwa wiki kwa udhamini wa Barrick.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad