HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, April 25, 2024

Stanbic Tanzania na Ramani kushirikiana kimkakati kuboresha sekta ya biashara nchini

Benki ya Stanbic Tanzania, ambayo ni kiungo muhimu katika sekta ya huduma za kibenki nchini Tanzania, na Ramani, kampuni namba moja kwenye teknolojia ya kifedha, wanafurahi kutangaza ushirikiano uliolenga kuleta mabadiliko kwenye sekta ya biashara, nakuendeleza upatikanaji wa huduma za kifedha nchini  kwa ufanisi zaidi. 

Ushirikiano huu wa kipekee unalenga kutumia teknolojia na msaada mkubwa wa kifedha, kuimarisha uwezo wa biashara za wasambazaji wa ndani na wajasiriamali.

Muunganiko huu unalenga kutumia miundombinu yakifedha ya kisasa ya Kampani ya Ramani, pamoja na rasilimali imara za kifedha za Benki ya Stanbic.

Pia, utasaidia zaidi ya wasambazaji 100 katika mwaka wake wa kwanza, ukiangazia mnyororo muhimu wa thamani katika sekta ya Bidhaa za Watumiaji (FMCG). 

Pamoja na majukwaa ya teknolojia ya hali ya juu na mikakati ya kifedha, ushirikiano huu utakabiliana na vipengele muhimu vya usimamizi wa biashara, ufuatiliaji wa mauzo, na miamala ya kidijitali ili kuongeza ufanisi wa uendeshaji kwa wasambazaji.

Fredrick Max, Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benkiya Stanbic Tanzania, alisema, "Ushirikiano wetu na Ramani ni zaidi ya biashara; ni ushirikiano wa kimkakati ambao unaahidi kubadilisha jinsi biashara inavyofanywa nchini Tanzania. 

Kwa kuunganisha nguvu zetu na maono yetu, tunapanga kusaidia mahitaji ya kifedha ya wasambazaji wa ndani, na pia kuchangia kwa kiasiki kubwa katika ukuaji wa uchumi wa taifa letu."

Lengo kuu ni kutoa fedha kwa wasambazaji na wauzaji ili kuboresha usimamizi wa ugavi kwa wasambazaji na wafanyabiashara wa bidhaa kubwa. 

Hii itawezesha usimamizi bora wa manunuzi, udhibiti wahisa na ufuatiliaji wa mauzo ya kidijitali katika kuimarisha michakato ya biashara na miamala yakifedha.

Iain Usiri, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampani ya Ramani, alisema, "Tunafurahi kushirikiana na Benki ya Stanbic Tanzania. Ushirikiano huu utarahisisha na kuimarisha usimamizi wa wasifu wa mikopo na kukuza huduma za kifedha.  Tunable mabadiliko chanya katika kuendesha biashara, na kuboresha upatikanaji wa huduma za kifedha."


Mafanikio ya ushirikiano huu yatapimwa nauandikishwaji wa wafanyabiashara 100 katika mwaka wakwanza, na mipango ya kukuza ufikiaji kwa kiasikikubwa, ili kufikia biashara zaidi nchini Tanzania.

Takwimu za mitandao ya kijamii, ukuaji wa kifedha, naviwango vya kuandikisha wateja, zitatumika kamaviashiria muhimu vya mafanikio na ufanisi wamuunganiko huu.

Ushirikiano kati ya Benki ya Stanbic Tanzania na Ramani, unatengeneza kiwango kipya cha ushirikiano katika sekta ya kifedha na teknolojia, huku ukionyeshamatumaini makubwa katika kuboresha jinsi biasharainavyofanywa na kusaidiwa kifedha nchini Tanzania.

Kupitia hatua hii, mashirika yote mawili yanathibitishatena azma yao ya kuchochea ukuaji wa kiuchumi, nakuboresha upatikanaji wa huduma za kifedha kwaWatanzania wote.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad