Katika kuunga mkono makundi mbalimbali na kurudisha kwa jamii, KCB Bank Tanzania imedhamini na kushiriki mbio fupi za hisani za Run4Autism Tanzania zenye lengo la kuongeza uelewa juu ya tatizo la usonji nchini.
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa
akiwa kama mgeni rasmi, alitoa pongezi za kwa Benki ya KCB Tanzania kwa
kuendelea kuunga mkono makundi jitihada mbalimbali kupitia uwekezaji kwa
jamii.
Mkuu
wa Idara ya Masoko, Uhusiano na Mawasiliano, Christina Manyenye
akimuwakilisha Mkurugenzi wa Biashara wa Kanda wa KCB Group na
Mkurugenzi Mtendaji wa KCB Bank Tanzania, alisisitiza kuwa mbali na
mafunzo ya ujuzi na ufundi ya 2jiajiri, KCB Bank Tanzania itaendelea
kutekeleza azma yake ya kuigusa jamii na makundi mbalimbali kwa namna
tofauti.
“KCB
Bank tunaungana na Lukiza Foundation katika kuleta elimu ili wazazi
wengi wajitokeze na kuwasaidia Watoto wenye tatizo la usonji nchini,
tunaamini kupitia mbio hizi tunachangia katika kuleta mabadiliko Chanya
kwa manufaa ya jamii yetu, alisema.
Kupitia
mbio hizi, benki imeonesha dhamira yake ya kuunga mkono jitihada za
kuongeza ufahamu wa ugonjwa wa usonji na kuendeleza michezo nchini.
Mbali
na hilo, benki ya KCB inashiriki katika masuala mbalimbali ya
kimaendeleo ikiwamo kusaidia vijana kielimu na kiujuzi kupitia program
ya 2jiajiri ambayo imekuwa chachu katika kupunguza tatizo la ajira.
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa
akimkabidhi cheti cha udhamini Mkuu wa Masoko, Mawasiliano na Uhusiano
wa KCB Bank Tanzania, Christina Manyenye wakati wa mbio za usonji
(Run4Autism Marathon) zilizofanyika siku ya Jumapili jijini Dar es
Salaam.
1.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa
Majaliwa akiwa na viongozi mbalimbali, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu na
viongozi mbalimbali akiwamo Mkuu wa Masoko, Mawasiliano na Uhusiano wa
KCB Bank Tanzania, Christina Manyenye wakati wa mbio za usonji
(Run4Autism Marathon) zilizofanyika siku ya Jumapili jijini Dar es
Salaam.
No comments:
Post a Comment