HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, April 22, 2024

DC MPOGOLO AONGOZA MAOMBEZI YA TAIFA KATIKA HALMASHAURI YA JIJI LA DAR

 








*Jiji la DSM lafanya Hafla ya Maombi na Dua ya Kuliombea Taifa

KTIKA kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanzania leo tarehe 22, Aprili 2024 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeandaa Maombi na Dua ya kuliombea Taifa yaliyofanyika katika Ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es Salaam yalioambatana na kauli mbiu isemayo “Tumeshikamana na Tumeimarika kwa maendeleao ya Taifa Letu”.

Akiongoza hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo ameeleza kuwa “ tumeandaa Maombi na Dua ya kuliombea Taifa letu ikiwa ni sehemu ya Kumshukuru Mungu kwa kufikisha miaka 60 ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa amani kwani kama Taifa tumeshikamana na tumeimarika kwa miaka 60 hivyo hatuna budi kufanya Maombi na Dua kwaajili ya kuendelea kuimarisha amani ya nchi yetu”.

Sambamba na hilo Mhe. Mpogolo ameendelea kusema “katika maombi na Dua hizi tunaendelea kumuombea Rais wetu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anayoifanya ya kuendelea kuimarisha Muungano kwa amani pamoja na kuhakikisha nchi yetu inaendelea kupata maendeleo bila kusahau kuombea uchaguzi wa Serikali za mitaa unaoenda kufanyika Octoba 2024 ufanyike kwa Amani na tupate viongozi bora zaidi watakaoendelea kutuletea maendeleo.”

Kwa upande mwingine Mhe. Mpogolo amewahakikishia Wananchi wa Wilaya ya Ilala kutatua changamoto ya Athari za mvua kwani tayari ashawaelekeza wataalamu kutoka TARURA wakiambatana na Wahandisi kutoka Jiji la Dar es Salaam kutambua maeneo yote yaliyoathiriwa na mvua ili pindi mvua zitakapopungua maeneo hayo yatafanyiwa marekebisho.

Aidha kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam Ndg. Jomary Satura ameahidi kuendelea kushirikiana na viongozi wa dini kuliombea Taifa letu huku akiwahakikishia kushirikiana na watendaji wake kutatua kwa wakati changamoto zinazowakabili wananchi wa Wilaya ya Ilala kama Mheshimiwa Rais anavyoelekeza.

Akitoa Shukrani zake kwa viongozi wa Dini walioshiriki kuliombea Taifa Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto ameeleza kuwa “kupitia Maombi na Dua hizi za kuliombea taifa kufikisha miaka 60 ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ni Imani yangu maombi haya yatadumisha Amani na yatakuwa chachu ya maendeleo kwa nchi yetu”.

Naye Sheikh wa Wilaya ya Ilala Adam Mwinyipingu ameipongeza Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kuandaa siku ya Maombi na Dua ya kuliombea Taifa kwaajili ya muungano kwani maombi haya ni sehemu ya uzalendo pamoja na mshikamano kwa viongozi huku akiahidi kusimama na kuimarisha Muungano wa Tanzania kupitia Dua na Sala ili nchi iendelee kuwa na amani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad