Mbali ya kuhani msiba huo, Katibu Mkuu wa CCM Balozi Dk. Nchimbi pia alipata wasaa kwenda kumsalimia Bi. Ruth Kabula Bogohe, mstaafu mwenye miaka 88, ambaye aliwahi kuwa Mjumbe wa NEC ya CCM Taifa kwa miaka 15, Mwenyekiti wa UWT kwa miaka 10 na Katibu Tarafa maeneo mbalimbali nchini kwa miaka 25.
Viongozi wengine waliombatana na Balozi Dk. Nchimbi, ni pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Komredi Michael Lushinge (Smart), Mjumbe wa NEC Taifa, Komredi Richard Kasesera, Katibu wa Mkoa wa Mwanza, Komredi Omari Mtua, Mjumbe wa NEC Mkoa wa Mwanza, Komredi Jamal Babu na Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Ndugu Amina Makilagi (kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza).




No comments:
Post a Comment