HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, March 30, 2024

BODABODA MAGOMENI WANUFAIKA NA MERIDIANBET



MABINGWA wa michezo ya kubashiri kampuni ya Meridianbet mapema leo imefika eneo la Magomeni jijini Dar-es-salaam na kufanikiwa kutoa msaada kwa madereva Bodaboda wa eneo hilo.

Bodaboda wanaofanya shughuli zao kila siku katika eneo la Magomeni wamejikuta wakinufaika kutokana na Meridianbet kufika eneo hilo, Kwani hawakwenda mikono mitupu walikwenda kugawa Reflectors kwa madereva hao kwajili ya usalama wao wa barabarani.

Lengo La Meridianbet kutoa Reflectors kwa Bodaboda kwajili ya kuhakikisha wanaungana na Serikali katika kuhakikisha wanapunguza ajali barabarani,Kwani kupitia Reflectors imekua ikiwasaidia sana Bodaboda kuepukana na ajali za mara kwa mara barabarani.

Aidha mkuu wa kitengo cha mawasiliano na masoko kutoka Meridianbet Bi. Nancy Ingram alipata nafasi ya kuzungumza katika eneo hilo akiiwakilisha taasisi ya Meridianbet “Kwanza kabisa nipende kuwashukuru viongozi wa eneo hili kuweza kufanikisha sisi kufika hapa, Lakini jambo la msingi ni furaha yetu kuona tunaungana na serikali katika kupiga vita ajali za barabarani kwa kuweza kufika hapa na kugawa Reflectors”

Suka mkeka wako kwenye michezo mikali itakayopigwa leo kwenye ligi mbalimbali barani ulaya na dunia kwa ujumla. Machaguo zaidi za 1000 yapo huku lakini vile vile Turbo Cash pia ipo. Unasubiri nini sasa? Ingia meridianbet na ubashiri sasa.`

Kiongozi wa Umoja wa Bodaboda eneo la Magomeni nae alipata nafasi ya kuongea baada ya Meridianbet kufika eneo hilo na kutoa neno la shukrani “Tunashukuru sana kwa kampuni hii kongwe kabisa kufika eneo hili na kuweza kutoa msaada wa Reflectors kwetu ambazo kiukweli zitakwenda kutusaidia sana kuepusha ajali za barabarani ambazo tumekua tukikumbana nazo mara kwa mara, Nipende kutoa wito kwa makampuni mengine yaweze kujitoa na kugusa jamii kama Meridianbet”

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad