HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, January 18, 2024

WATANZANIA WAHIZIMIWA KUTAFUTA FURSA ZA KIBIASHARA KWA KUTUMIA SIMU JANJA

 





WATANZANIA wamehimizwa kujikita katika matumizi ya simu janja ili kutafuta fursa za kibiashara hatua ambayo itasaidia kuondokana na ombwe la utegemezi kwa serikali pamoja na jamii inayowazunguka.

Kauli hiyo imetolewa Jijini Dar es salaam na Mkuu wa kitengo cha biashara ya simu za mkononi ya Samsung Tanzania, Mgope Kiwanga wakati wa uzinduzi wa simu mpya lengo ni kuleta uchechemuzi wa kibiashara.

Amesema pamoja na mambo mengine Samsung Tanzania imetenga fedha ili kuwawezesha wafanyabiashara mtandao kwa kutumia simu janja ili kuongeza ufanisi wa biashara kwa wafanyabiashara wadogo na wakati –SME’s.

‘’Kitu ambacho kinatutofautisha sisi na wengine wote Samsung tunatoa simu za mkopo kupitia washirika wetu kama vile kampuni za mawasiliano ikiwemo Tigo na Vodacom kwahiyo wananchotakiwa ni kuwa waaminifu’’ Alisema Kiwanga.

Aidha amesema simu hizo ni Galaxy S24 Ultra, Galaxy S24 ambapo amesema hatua ya kuzinduliwa simu hizo kwa pamoja Duniani kote ni urithi wa uvumbuzi.

Kampuni ya Samsung imesema zoezi la kuanza kuagiza simu hizo mpya kwa upande wa Tanzania litaanza Januari 18 hadi Februari 13 mwaka huu pamoja na kutoa zawadi mbalimbali.

Imeelezwa kuwa simu janja za Galaxy S24 pamoja na nyingine zilizozinduliwa zimetajwa kuchochea ubunifu wa matumizi ya vifaa vya kidigitali vinavyotumia teknolojia.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad