"Vifaa hivi vimetolewa na Msamaria Mwema aliyetamani sadaka yake ifike kwa watoto wanaozaliwa Njiti katika Hospitali hii, baada ya kumuelezea namna ambavyo wanapata changamoto kuwapatia rufaa wakina Mama kwenda katika Hospitali zingine" Doris Mollel
"kwa vifaa hivi tutaanza huduma mapema kabla ya mwaka haujaisha, tutapunguza sana rufaa kwenda Mwanyamala na Muhimbili." Dkt. Tulitweni Mwinuka Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ubungo.
Kwa Upande wake Daktari wa Watoto Dkt. Edith Shirima amebainisha kuwa huwa wanawapa rufaa watoto 10 mpaka 16 kwa mwezi kwenda Hospitali ya Mwananyamala au Muhimbili kwa ajili ya huduma hiyo.







No comments:
Post a Comment