HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, September 8, 2023

McF kufanya jitihada za kuzuia Vifo na Ulemavu vinavyohusiana na ujauzito na watoto walio na umri chini ya miaka mitano.


 Na Mwandishi wetu

Shirika lisilo la kiserikali Maternal Care Foundation ( McF) limeendelea kufanya jitihada za kuzuia Vifo na Ulemavu vinavyohusiana na ujauzito miongoni mwa wanawake na watoto chini ya umri wa miaka mitano.

Lengo ikiwa ni kuboresha mazingira ya afya katika afya ya uzazi, na mtoto mchanga.

Akizungumza wakati wa maonyesho ya afya ya wanawake yaliyofanyika tarehe 2 Septemba 2023 katika viwanja vya maonesho Mliman city Afisa Mkuu wa Habari  wa McF, Bw. Tesha Mbiligili amesema wameendelea kusisitiza umuhimu wa uhamasishaji wa jamii, elimu, na upatikanaji wa huduma za afya kwa ajili ya kufikia matokeo bora  ya afya lakini pia kuona haja ya kuwepo mbinu shirikishi kwa afya ya mama na mtoto.

"Katika hafla hii ilitolewa elimu ya afya bila malipo, huduma za upimaji na uchangiaji damu ili kushughulikia masuala muhimu yanayoathiri afya ya mwanamke na watoto chini Tanzania."

"Hafla hii imeonyesha nguvu ya ushirikiano na ari ya mashirika haya katika kuboresha maisha ya wanawake na watoto nchini Tanzania." Amesema Bw.Tesha


Amesema kwa kuzingatia kukuza afya ya uzazi, afya ya akili, ukuaji wa watoto, afya ya uzazi na lishe, hafla hiyo imeleta pamoja mashirika mbalimbali ambapo kila mmoja alichangia utaalimu wake ili kuinufaisha jamii.

"Washirika wakuu katika maonyesho hayo ni pamoja na, Shujaa Cancer Foundation, Nursing and Midwifery Empowerment Organization, Mental Health Tanzania, Tanzania Epilepsy Organization, Watoto Afrika, Bright Jamii Initiative, Kaya Foundation, Gorgeous Look Atelier, Hospitali ya CCBRT na Hospitali ya Sanitas."

"Maonyesho ya Afya ya Wanawake yalikuwa tukio la uzinduzi ambalo linaonyesha dhamira kuu ya McF ya kuboresha matokeo ya afya kwa wanawake na watoto. Hili lilikuwa jukwaa la kuwawezesha wanawake na watoto kwa taarifa sahihi za afya na rasilimali muhimu, na kuwawezesha kufanya maamuzi sahihi ya afya. Mpango huu unaondoa vikwazo vinavyozuia upatikanaji wa taarifa muhimu za afya ndani ya jamii." Amesema Bw.Tesha

Kadhalika Bw.Tesha amesema McF inaendelea kufanya mawasiliano na jamii, kushirikiana na washikadau katika sekta ya afya, na kutoa elimu bila malipo kwa jamii ili kuboresha matokeo ya afya ya uzazi.

 

 **********************

 









 

1 comment:

Post Bottom Ad