Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi, Dkt Yose Mlyambina amewataka watumishi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi kutumikia jamii ya Tanzania kwa uaminifu na haki wakati wa utatuzi wa migogoro ya kikazi.
Aidha, amesema wanapaswa kuwa watu wenye hekima pindi wanapotekeleza majukumu ya Tume, kufanya hivyo wataongeza imani kwa wananchi.
Ameyasema hayo Septemba 27, 2023 Jijini Dar es Salaam wakati wa Uapisho wa Mkurugenzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) iliyofanyika katika Ukumbi wa Mahakama ya Kazi.
Sambamba na hayo, Dkt. Mlyambina amesema Watumishi wa Tume pamoja na Mahakama wana wajibu mkubwa wa kuelimisha jamii kuhusu usuluhishi na kuhakikisha kuwa mashauri mengi yanatatuliwa kwa njia ya usuluhishi.
Naye, Mkurugenzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Mhe. Usekelege Mpulla ameishukuru Bodi ya Tume, Menejimenti pamoja na Watumishi, amehaidi kushirikiana nao katika utekelezaji wa majukumu ya Tume.
Vilevile, Mhe. Mpulla amesema migogoro inayohusu wafanyakazi na waajiri inapaswa kufanyiwa kazi haraka na kwa wakati ili kukuza uchumi wa Nchi.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjcP8dysuqJWa0qlyHfg3AbyETJAh4kzCHhIm7lZT7mrjUT41Ssg4p84JKD_szQHtjrdj_WiyEEoi3RFnzt8nFa7ho1muWrwSoXXXuFufQv_2hF0mHKcgtp3_X_NBdLmvGUox-uqFHrbZouiHfm2KbrIbIituQ2ygJcDtGggTIKxZzUab4Y_vl97zNFBu8/w640-h426/WhatsApp%20Image%202023-09-28%20at%2001.02.34%20(1).jpeg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEga0QpC6MQG3n51ryiv0M1qj0njgKfbBuPMheYh_TuUqvqjkLLMwKyeZv2rZYmkgeoOrxfzhJisGoM7aEfYSVYqn3h2fot8oB-xtJnFnqFNieuNPu2Qq7gSUmPrdffurJNYy5xqhugzsRmfPruo7qlppQaTHr6o82iHONodd4W6I781MEfXSfEh1OHqG04/w640-h426/WhatsApp%20Image%202023-09-28%20at%2001.02.34.jpeg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg_CGJ3GSxBvHhYnSmvLCrmLxoXPulF9LCMv4XZoRtokSpYCYCWvRTLhLiaOYPvNEAmztraD1Qjr8bzkNpJD0b036POEV4_29BekQjXLo364Czj9kvo1Z94K1paGvwmMKJafKeKG_CdGKQslYc3xGmChlolfkMtJMGZjWiEQht9aeti_9BQLQgS2utnnSQ/w640-h498/WhatsApp%20Image%202023-09-28%20at%2001.02.35.jpeg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjU1_HD672vBwPvGMVTCBWsqWEjCoyr9dqoEDJfqAiUcQGIFcoAdkug0IVN9XqzevKFM4D4gJTLdUL_JhANiVRE1cDWokXKrDFwQV_7ncUXUj3ZG2WJnmmLpfeeQwgwj6oGr6q2ibBYTcYSrpbtd-wZFSsZ0BLo733VCulc85VNWaUtaq334_N3WeQbxHU/w640-h426/WhatsApp%20Image%202023-09-28%20at%2001.02.35%20(1).jpeg)
No comments:
Post a Comment