Mkuu
wa Idara ya Mauzo NMB Bw.Donatus Richard akizungumza katika ufunguzi na
kuchezesha droo ya kwanza ya Kampeni ya 'BONGE LA MPANGO , MOTO ULE
ULE' awamu ya tatu iliyofanyika leo Aprili 13,2023 Jijini Dar es Salaam.
Mkuu
wa Idara ya Mauzo NMB Bw.Donatus Richard akizungumza katika ufunguzi na
kuchezesha droo ya kwanza ya Kampeni ya 'BONGE LA MPANGO , MOTO ULE
ULE' awamu ya tatu iliyofanyika leo Aprili 13,2023 Jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi
kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania Bw.Elibariki Sengasenga
(kulia) akizungumza katika ufunguzi na kuchezesha droo ya kwanza ya
Kampeni ya 'BONGE LA MPANGO , MOTO ULE ULE' awamu ya tatu iliyofanyika
leo Aprili 13,2023 Jijini Dar es Salaam.
NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV
BENKI
ya NMB imefungua na kuchezesha droo ya kwanza ya Kampeni ya 'BONGE LA
MPANGO , MOTO ULE ULE' na kuwapata washindi ambao wamejishindia pikipiki
pamoja na fedha tasilimu ya shilingi laki mbili kila mmoja.
Katika
ufunguzi wa Kampeni hiyo ambayo imefanyika leo Aprili 13,2023 katika
Makao Makuu ya NMB Jijini Dar es Salaam, wametangazwa washindi wawili
kutoka maeneo tofauti ambao ni Stella Meleck Mafuwe kutoka Babati ambaye
amejishindia pikipiki ya shilingi milioni tatu na wa pili ni Mushema
Deocles Muganyizi kutoka Mwanza ambaye amejinyakulia pesa tasilimi
shilingi laki mbili.
Akizungumza
na waandishi wa habari kwenye ufunguzi wa kampeni hiyo, Mkuu wa Idara
ya Mauzo NMB Bw.Donatus Richard amesema zawadi ambazo waliziandaa kwa
wateja watakaofungua na kuweka akiba kwenye Benki ya NMB kuanzia
shilingi Laki moja (100,000/=) nakuendelea kunafaida ambazo atajishindia
ikiwemo pesa taslimu, pikipiki ya miguu mitatu, pikipiki za miguu
miwili pamoja, friji ya milango miwili, TV janja, Simu ya mkononi,
Laptop, mashine ya kuulia nguo na zawadi nyingine nyingi.
Amesema
Kampeni hii ya Bonge la Mpango awamu ya tatu inajumuisha wateja wote wa
NMB kwa sasa na wale watakaofungua akaunti mpya ya NMB.
"Hata
hivyo kwenye Kampeni hii kutakuwa na zaidi ya shilingi milioni 180
zitakazotolewa kama zawadi kwa washindi 100 lakini pia kwenye kampeni
hiyo itakayoendeshwa ndani ya wiki 12 kila wiki tutapata washindi 12
watakaopokea shilingi laki moja kila mmoja pia kutakuwa na mshindi mmoja
kila wiki atakaejishindia shilingi laki mbili na vilevile kutakuwa na
mshindi kila wiki atakaekuwa anajishindia pikipiki". Amesema
Aidha
amesema Washindi watano watajinyakulia shilingi milioni moja kwa kila
mwezi kwa kila mtu na katika kuhitimisha kampeni hiyo kwenye fainali
watakuwa na washindi 11 watakaojumuisha vitu vifuatavyo kama pikipiki,
bajaji za mizigo na wengine 7 watajishindia vifaa vya kielektroniki kama
friji ya milango miwili, TV janja, Simu janja za Iphone 14, laptop na
mashine za kufulia nguo .
Kwa
upande wake Mwakilishi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania
Bw.Elibariki Sengasenga ameipongeza NMB kwa kuandaa kampenihiyo kwani
toka mwanzo wamekuwa wakitoa ushirikiano mzuri mpaka hadi sasa kuelekea
kampeni ya Bonge la Mpango.
Pamoja
na hayo amewataki ushiriki mwema wale wote watakaoshiriki kwenye
kampeni hiyo ambayo imeanza na kuwapata washindi ambao watapewa zawadi
zao.
No comments:
Post a Comment