Na Mwandishi Wetu,Michuzi TV
KAMPUNI
ya Gf Truck & Equipments Lt kupitia kampuni yake ya ukodishaji wa
mitambo ya RENTO MACHINE wamesaini makubaliano na Shirika la Madini
nchini (STAMICO)kwa ajili ya kuwasaidia na kuwainua wachimbaji wadogo wa
madini ili kuongeza pato lao na pato la taifa.
Pia
imeelezwa kwa kufanya hivyo kutaongeza morali kwa wachimbaji wadogo
ambao hawana uwezo wa kununu mashine hizo za kuchimbia huku ikielezwa Gf
Trucks & Equipment’s ambao ni wauzaji wa mitambo ya kuchimbia ya
XCMG na AJAX wanautaratibu wa kuwakopesha wakandarasi wadogo wa miradi
mbali mbali ya serikali kwa dhamana na mtambo husika kupitia beki rafiki
ambayo Mkandarasi mwenye mradi anaweza akakopesha vitendea kazi na
akalipa kwa awamu.
Akizungumza
leo Aprili 5,2023 wakati wa kusaini makubaliano hayo Mkurugenzi wa
Masoko na Mawasiliano wa Kampuni ya GF Salman Karmali amesema wamegundua
wachimbaji wengi wadogo hawana mitaji ya kununua mitambo hiyo na
kutokana na hilo wameamua kuingia makubaliano na STAMICO S ya
kuwakodisha mitambo maalumu ya kuchimbia kwa gharama nafuu .
"STAMICO
kama walezi wa wachimbaji madini nchini ni rahisi kumtambua mhusika
mwenye mahitaji na kwa kufanya hivyo tutapunguza ajali nyingi
zinazotokea migodini kwa wachimbaji kutumia njia za asili , hivyo sasa
tumekuja kama mkombozi wao kupitia XCM na AJAX tutakua tumetatua
changamoto zao kwa kiwango kikubwa."
Kwa
upande wake Naumu Mwakasita akizungumza kwa niaba ya wachimbaji wadogo
amesema wao wameichukulia hiyo kama fursa inayokuja kuwakomboa na hali
ya kutumia vifaa duni katika uchimbaji, hivyo yeye atakuwa wa kwanza
kuchangamkia fursa hiyo na kuachana na uchimbaji kwa kutumia njia za
asili ambazo ni hatari
Wakati
huo huo Waziri wa Madini Dotto Biteko amewataka wachimbaji
kuchangamukia fursa ya kutumia mitambo hiyo kwani inakwenda kuongeza
thamani ya madini na kuweza kupata madini yenye ubora. “Ninazo taarifa
wachimbaji wengine wamekuwa wakichanganya na vitu vingine ili kuongeza
uzito, mfano unachimba gympsum umeshaipata lakini unaamua kuchukua
mchanga usiokuwa na thamani yoyote ili kuongeza uzito wa mzigo wako,”
amesema.
Amesema
kwa kufanya hivyo wamekuwa wakiwatia hasara wenye viwanda jambo ambalo
linaweza kuwafanya kufilisika, kufunga viwanda na kuwafanya wao kama
wachimbaji wakose soko.“Kuweni waaminifu, kama hauiogopi Serikali basi
muogope Mungu, hakuna mtu mwenye akili yake timamu anayeweza kuagiza
malighafi kutoka nje kama hiyo malighafi anapata hapa nchini kwa bei
nafuu na safi."
Waziri
Biteko amesema kumekuwepo na malalamiko kutoka kwa wachimbaji wakieleza
kupunjwa fedha na wenye viwanda kwa kukatwa baadhi ya tani na wanunuzi
kwa kuhofia kuwa zitakuwa na takataka.“Kama mtu amepeleka gari lake la
tani 30, tani 3 zinakatwa na kuhesabiwa kama ni uchafu, wanampunja
mchimbaji kuanzia kwenye uzito na wakati mwingine katika kutumia bei
elekezi.
Aidha
amesema ni vyema kuwapo kwa ushirikiano thabiti kwani sekta ya madini
ya viwandani ni moja kati ya zinazokuwa kwa kasi, ndani ya miaka miwili
ya Rais Samia Suluhu Hassan, mapato yake yamefikia Sh.trilioni 1.19
kutoka Sh.milioni 456.
Waziri
wa Madin, Dotto Biteko akimpongeza na kumkabidhi chet Mkurugenzi wa
Masoko na mawasiliano wa kampun ya GF, Salman Karmali baada ya kusaini
mkataba na STAMICO wa kuwakodisha mitambo ya kuchimbia madini wachimbaji
wadogo nchini wakati wa mkutano wa wachimbaji wadogo wa madini jijini
Dar es salaam
Mkurugenzi
wa Masoko na mawasiliano wa kampun ya GF, Salman Karmali akibadilishana
nyaraka na Mkurugezi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO)
Dkt. Venance Mwasse baada ya kusaini mkataba wa kuwakodisha mitambo ya
kuchimbia madini wachimbaji wadogo nchini wakati wa mkutano wa
wachimbaji wadogo wa madini jijini Dar es salaam jana.Kushoto ni Afisa
Mauzo wa kampuni ya GF Trucks & Equipment’s Ltd , Peter William
No comments:
Post a Comment