HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, March 27, 2023

NAIBU WAZIRI KASEKENYA AKAGUA MIUNDOMBINU YA BARABARA YA MIKA – UTEGI – SHIRATI NA MASONGA KIRONGWE KM 56, WILAYANI RORYA

 

Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Juma Chikoka akizungumza na Naibu Waziri wa Ujenzi Eng. Godfrey Kasekenya, kuhusu umuhimu wa barabara ya Mika – Utegi – Shirati na Masonga Kirongwe (km 56), iliyopo wilayani humo. Barabara hiyo pia inaunganisha mkoa wa Mara na nchi jirani ya Kenya.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya, akizungumza na Mbunge wa jimbo la Rorya, Mhe. Jafari Chege na Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Juma Chikoka wakati alipoikagua barabara ya Mika – Utegi – Shirati na Masonga Kirongwe (km 56) iliyopo wilayani humo. Barabara hiyo pia inaunganisha mkoa wa Mara na nchi jirani ya Kenya.
Mbunge wa jimbo la Rorya, Mhe. Jafari Chege, akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya, wakati alipoitembelea na kukagua barabara zilizopo jimboni mwake, Mkoani Mara
Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya, akiongozana na Mbunge wa jimbo la Rorya, Mhe. Jafari Chege pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Juma Chikoka wakati wakikagua barabara ya Mika – Utegi – Shirati na Masonga Kirongwe (km 56) iliyopo wilayani Rorya. Barabara hiyo pia inaunganisha mkoa wa Mara na nchi jirani ya Kenya.

 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad