HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, February 16, 2023

Pool kumpaisha Abdallah Hussein mpaka China

MCHEZAJI wa Pool wa timu ya TaifaAbdallah Hussein kutoka Klabu ya Snipers yenye makazi yake Mwenge Mpakani, Dar es Salaam, ameteuliwa na Chama cha Pool Taifa kuiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya Duniayanayotarajiwa kufanyika nchini China, yajulikanayo kama“World Heyball Championships 2023”.

Uteuzi wa Hussein umekamilika leo Februari 16 baada yamchakato uliofanywa na viongozi wa chama hichoakibebwauwezo mkubwa alioonyesha katika mashindano kadhaayaliyopita pamoja na kuwa na hati ya kusafiria (Passport).

Mwenyekiti wa Chama cha Pool, Isaac Togocho, amesema Hussein ataambatana na kiongozi mmoja wa chama hichoambaye atamteua hivi punde.


Mashindano hayo yanatarajiwa kuanza rasmi Machi 21 – 27,2023 kwa hatua ya awali ya kufuzu na Machi 28 ni sherehe zaufunguzi rasmi wa fainali zenyewe zitakazoanza siku inayofuatana kuhitimishwa Aprili 5,2023.

1 comment:

Post Bottom Ad