Baraza La Biashara Afrika Mashariki (EABC) limewateua waTanzania 3 kuwa mabalozi wa Baraza hilo nchini.
Hii ni kuhakikisha baraza hilo linatimiza wajibu wake ipasavyo na kufanya biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na nchi za Afrika Mashariki zinashamiri bila vikwazo.
Baraza limewateua
Raphael Maganga - Mtaalamu wa Diplomasia ya Uchumi TPSF
Ms. Mercy Sila - Mwenyekiti wa Tanzania Women Chamber of Commerce
Dr. Samuel Nyantahe - Mkurugenzi Mtendaji Daima Associates
EABC iliundwa 1998, kama kiungo muhimu katika mkataba wa Jumuiya Ya Afrika Mashariki (EAC Treaty) Ambao ulilisisitiza ushiriki wa sekta binafsi ili kufikia maendeleo enedelevu ya kijamii, kiuchumi na kisiasa. Baraza hill ndio mwamvuli wa vyama vyote vya biashara katika nchi zote 7 za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
No comments:
Post a Comment