Halotel ikiwa kampuni
inayosifika nchini kupitia huduma zao za kifedha za HaloPesa, inaendelea
kuwahamasisha wateja wao kwa kuleta huduma za ubora na zenye ubunifu,
na wakizindua kampeni ya SHINDA TENA NA HALOPESA leo.
Wakiwa
kampuni inayokua kwa kasi sana HaloPesa, imeendelea kutoa huduma za
kifedha kwa wateja wao na wanaendelea kuja na huduma mbalimbali zenye
gharama nafuu ambazo zinafika kote mjini na kijijini Tanzania.
Akiongea
kwenye mkutano wa waandishi wa habari katika ofisi za Halotel Tanzania,
Naibu Mkurugenzi Mkuu Bw: Magesa Wandwi alisema “Huwa tunafuraha kubwa
kutoa huduma hizi za kifedha, na kuwawezesha wateja hususani wateja wa
HaloPesa kufanya miamala tofautitofauti kama kutuma pesa kwenda
HaloPesa, kutuma pesa kwenda mitandao mengine, kutuma pesa kwenda benki,
kulipia billi, Lipa hapa nakadhilika. Zaidi ya wateja 2.5m ambao ni
wateja hai wanaendela kufurahia huduma zenye ubora na kwa gharama nafuu
muda wowote.
Kampeni ya Shinda Tena na HaloPesa ni kwa ajaili ya
kuhamasiha na kuwapa motisha wateja wa HaloPesa ili waweze kuendelea
kutumia huduma zetu lakini pia kuwapa chachu wateja ambao hawatumii
huduma hizi za kifedha za kidijitali waweze kuingia kwenye ulimwengu
huu. Ni ndoto yetu kuona watanzania wote wanatumia huduma za kifedha
kiganjani mwao. Aliongezea Magesa
Kampeni ya Shinda na HaloPesa
ni kwa ajili ya wateja wa HaloPesa ambayo itakuwepo kwa miezi mitatu (3)
na jumla ya wateja 135 watakuwa washindi. Ambao wateja 120 watashinda
pesa Taslimu na wateja 12 watashinda Luninga Janja na wateja watatu 3
watashinda Bajaj mpya. Tutakua na washindi wa kila siku ambao watashinda
pesa Taslimu na washindi wa kila wiki wa Luninga janja na washindi wa
kila mwezi ambao watashinda Bajaj.
Kila mteja wa HaloPesa
anaalikwa kushiriki kwenye promosheni hii kwa kufanya miamala ifwatayo;
Kutuma hela HaloPesa kwenda HaloPesa, Kutuma hela mitandao mengine,
kutuma hela benki, Malipo ya serikali, Lipa billi, Lipa Hapa, kutoa
kupitia wakala, kutoa hela kutoka ATM pamoja na miamala ya HaloYako.
Mteja ataongeza nafasi yake ya kushinda zawadi, hivyo tunawahamashisha
wateja wetu kufanya miamala mingi ili waweze kupata nafasi kubwa ya
kushinda zawadi hizi kabambe. Alisema Magesa.
HaloPesa
inafurahia kuzindua promosheni hii leo na itaendelea kufikiria njia
nyingine Zaidi za kufanya ulimwengu wa huduma za kifedha kupitia simu
kuwa bora Zaidi kwa ajili ya wateja wetu.
Naibu Mkurugenzi Mkuu Halopesa, Bw: Magesa Wandwi: akiongea na Waandishi wa Habari leo katika Uzinduzi wa Kampeni Mpya ya Halopesa iendayo kwa jina la Shinda Tena na HaloPesa ambayo itaendeshwa kwa muda wa miezi mitatu (3) na jumla ya wateja 135 watakuwa washindi. Jumla ya wateja 120 watashinda pesa Taslimu na jumla ya wateja 12 watashinda Luninga Janja na wateja watatu 3 watashinda Bajaji mpya. Tutakua na washindi wa kila siku ambao watashinda pesa Taslimu na washindi wa kila wiki wa Luninga janja na washindi wa kila mwezi ambao watashinda Bajaj.
Naibu Mkurugenzi Mkuu Halopesa, Bw: Magesa Wandwi: akiwa na Afisa Masoko Halopesa Roxana Kadio wakikata utepe mbele ya wandishi wa habari leo kama ishara ya Uzinduzi rasmi wa Kampeni Mpya ya Halopesa iendayo kwa jina la Shinda Tena na HaloPesa ambayo itaendeshwa kwa muda wa miezi mitatu (3) na jumla ya wateja 135 watakuwa washindi. Jumla ya wateja 120 watashinda pesa Taslimu na jumla ya wateja 12 watashinda Luninga Janja na wateja watatu 3 watashinda Bajaji mpya. Tutakua na washindi wa kila siku ambao watashinda pesa Taslimu na washindi wa kila wiki wa Luninga janja na washindi wa kila mwezi ambao watashinda Bajaj.
No comments:
Post a Comment