Na Mwandishi, Wetu Michuzi TV
MAMLAKA
ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) imezindua Shindano la Masoko ya
Mitaji kwa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu na Taasisi za Elimu ya Juu pamoja na
kutunuku vyeti kwa wahitimu wa kozi ya watendaji katika Masoko ya Mitaji
wanaokidhi viwango vya Kimataifa katika ukumbi wa Mikutano
Akizungumza
mbele ya wageni waalikwa na wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi huo
uliofanyika Desemba 7, 2022 jijini Dar es Salaam Ofisa Mtendaji Mkuu wa
Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana CPA Nicodemus Mkama amesema
Katika kutekeleza moja ya mikakati ya Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta
ya Fedha CMSA inatekeleza mkakati wa utoaji wa elimu kwa umma kwa lengo
la kuongeza uelewa na ushiriki wa wananchi kuhusu fursa zinazopatikana
katika masoko ya mitaji.
Amesema katika utekelezaji wa mkakati
huo CMSA inaendesha Shindano kwa Wanafunzi wa Vyuo vikuu na Taasisi za
Elimu ya Juu Yaani the Capital Markets Universities and Higher Learning
Institutions Challenge, kwa lengo la kuongeza uelewa na kuwajengea
vijana uwezo wa kushiriki katika masoko ya mitaji kwa kutumia njia ya
mitandao ya kielektroniki yaani simu za mikononi na intaneti.
"Shindano
hili linahusisha wanavyuo wa elimu ya juu kote nchini - Bara na
Visiwani kushirki na kujifunza kwa vitendo na nadharia fursa mbali mbali
za uwekezaji katika masoko ya mitaji.Mhe. Mgeni rasmi, shindano hili
utakalozindua leo tarehe 7 Desemba 2022 linatarajiwa kufungwa tarehe 31
Machi 2023 ili kutoa muda wa kutosha kwa wanafunzi kushiriki bila
kuathiri ratiba za masomo.
"Limegawanyika katika sehemu kuu
mbili, ambazo ni (shindano la maswali na majibu - Quiz Competition) na
(Shindano la kuandika Insha - Essay Competition).Kupitia shindano la
Maswali na Majibu (Quiz Competition), wanafunzi wanatakiwa kujibu
maswali 100 kwa kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano kwa njia ya
simu za mkononi, tovuti
"Ambapo mshiriki alitakiwa kujisajili kwa
kuandika taarifa zake muhimu, ikiwa ni pamoja na majina matatu; jinsia;
chuo; na kozi anayosoma, na kisha kufuata maelekezo mengine.Kupitia
shindano la pili la Kuandika Insha (Essay Competition), wanafunzi
watatakiwa kuandika insha kuhusu “Namna masoko ya mitaji yanavyotumika
kupata fedha za kugharamia miradi ya maendeleo na kuchochea ujenzi wa
uchumi shindani kwa maendeleo ya watu”.
Ameongeza isha hiyo
inatakiwa isizidi kurasa nne (4), maneno 1,500 na kisha kuituma insha
hiyo kwa barua pepe ambayo ni challenge@cmsa.go.tz. Washindi katika
mashindano hayo ni wale ambao watapata alama za juu kuliko washiriki
wengine na ambao pia wataweza kujibu kwa ufasaha maswali ya usaili
utakaofanyika mbele ya jopo la majaji ili kudhihirisha kuwa wao ni
washindi
Aidha amesema katika mwaka huu, CMSA imeweka lengo la
kuwafikia wanafunzi wapatao 18,000 ikilinganishwa na wanafunzi 16,275
walioshiriki shindano hili katika mwaka wa fedha 2020/2021, ikiwa ni
matarajio ya ongezeko la asilimia 10.6 na kwamba ili kufikia lengo hio
wameweka mikakati mbalimbali ya kurahisisha ushiriki wa wanafunzi ikiwa
ni pamoja na kuboresha mfumo wa teknolojia ya habari na mawasiliano kwa
kutumia njia ya simu za mkononi, tovuti, na barua pepe
Ambapo
mwanafunzi kwa kutumia bando lake la kifurushi cha kawaida ana uwezo wa
kuingia kwenye tovuti ya shindano na kupata taarifa na taratibu za
ushiriki na kuajiandikasha kushiriki katika shindano la maswali na
majibu na hali kadhalika kuwasilisha inshia yake. Kwa wanafunzi ambao
wako maeneo ambayo yana changamoto za mtandao wa kieletroniki bado
wataweza kushiriki shindano hili kwa kutumia barua pepe na simu za
mkononi kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi yaani “SMS”.
"Hivyo
basi, wanafunzi wanaweza kutumia simu janja (Smartphone) au kiswaswadu
(USSD). Mhe. Mgeni rasmi, ili kuwezesha washiriki wa shindano hili
kutumia elimu ya nadharia watakayoipata kwa vitendo, CMSA imeandaa
utaratibu wa kuwawezesha washiriki wa shindano hili kuwa wawekezaji
halisi.
"Kupitia mpango huu washindi 80 watakaopata alama za juu
kwenye shindano, watatumia theluthi moja ya zawadi ya fedha taslimu
watakazopata ili kuwekeza kwenye masoko ya mitaji kwa kununua hisa na
hatifungani za kampuni zilizoorodheshwa katika Soko la Hisa la Dar es
Salaam; au vipande katika mifuko ya uwekezaji wa pamoja.
"Mpango
huu unatarajia kuongeza wawekezaji wapya katika masoko ya mitaji.Mhe.
Mgeni rasmi, miongoni mwa zawadi watakazopata washindi wa shindano hili
ni kama zifuatavyo:Washindi wa kwanza kwa kila shindano kwa upande wa
wavulana na wasichana watapata Sh.1,800,000
"Washindi wa pili kwa
kila shindano kwa upande wa wavulana na wasichana watapata
Sh.1,400,000);Washindi wa tatu kwa kila shindano kwa upande wa wavulana
na wasichana watapata Sh.800,000
Washindi wa nne kwa kila
shindano kwa upande wa wavulana na wasichana watapata Sh.400,000);
Washiriki waliobaki katika 10 bora watazawadia Sh 200,000 .Washiriki
wote waliofika fainali na kuwa miongoni mwa washindi 20 walioshika
nafasi za juu watapatiwa vyeti (certificate of recognition); fulana
zenye nembo ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana;
Pia
Washiriki 6 wavulana; na 6 wasichana wenye alama za juu zaidi
watagharamiwa ziara ya kutembelea maeneo mbalimbali ili kujifunza zaidi
maswala ya masoko ya mitaji ikiwa ni pamoja na masoko ya hisa na kampuni
kubwa zinazohusika na utoaji huduma katika masoko ya mitaji hapa nchini
na nje ya nchi.
"Aidha hapa tunao baadhi ya wanafunzi washindi
wa shindano la mwaka 2020/2021 ambao wameweza kuendeleza ndoto zao za
kushiriki kwenye soko la mitaji na hivyo kutumia sehemu ya fedha zao
walizopata kama zawadi kununua hisa za kampuni mbalimbali
zilizoorodheshwa katika Soko la Hisa.
"Hawa sasa wamekuwa
wawekezaji halisi na sio kwa nadharia tu. Hawa pia, leo utawakabidhi
vyeti vya umiliki wa hisa zao walizonunua kwa kutumia fedha za zawadi ya
ushindi na wengine wameongezea fedha zaidi ya hizo na kununua hisa,
ambapo uwekezaji wao umekua kwa zaidi ya asilimia 300.Katika jitihada za
kuongeza idadi, ueledi na ufanisi wa wataalamu wa masoko ya mitaji
wanaokidhi viwango vya kimataifa wenye lengo la kukuza na kuendeleza
masoko ya mitaji hapa nchini,"
Ameongeza kwamba Mamlaka imekuwa
ikishirikiana na Taasisi ya Kimataifa ya Uwekezaji na Dhamana (Chartered
Institute for Securities and Investment - CISI) ya nchini Uingereza,
katika kuendesha mafunzo yanayotambulika kimataifa yanayolenga kujenga
uwezo na ufanisi kwa watendaji w"a masoko ya mitaji.
MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana(CMSA) Dk.John Mduma akizungumza jana jijini Dar es Salaam wakati akizindua shindano linalohusu masoko ya mitaji kwa wanafunzi wa vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu, ambapo Mamlaka ya Masoko wanatarajia washiriki wapatao 18,000 watashiriki Shindano hilo.
MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) Dk.John Mduma akipongezwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) CPA Nicodemus Mkama mara baada ya kuzindua shindano linalohusu masoko ya mitaji kwa wanafunzi wa vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu, ambapo Mamlaka ya Masoko wanatarajia washiriki wapatao 18,000 watashiriki Shindano hilo.
No comments:
Post a Comment