HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, November 28, 2022

 MKURUGEZI GF TRUCKS & EQUIPMENTS,IMRAN KARMAL ASHINDA TUZO YA CEO 2022

 
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya GF Trucks & Equipments Ltd, Imran Karmal ,amepata tuzo ya kuwa Mtendaji Mkuu Bora namba 2 wa mwaka 2022 wakati wa Tuzo zilizofanyika jijini Dar es salaam.

Tuzo hizo zilizoandaliwa na taasisi ya kimataifa ya KPMG kwa kwa kushirikiana na Tasisi ya Mameneja nchini Tanzania (Institute of Manager Tanzania )
Ushindi huo wa Karmal ni zawadi kwa wafanyakazi wote wa kampuni anayoiongoza ya GF Trucks & Equipment Ltd na furaha kwake kwani bila wafanyakazi imara hakuna kiongozi imara alimaliza Karmal.

Hii ni mara ya pili kwani mwaka jana alishika nafasi ya 9 kati ya CEO 100 waliokuwa wakiwania nafasi hiyo na tunashukuru mungu mwaka huu kuwa namba mbili wakati nafasi ya kwanza ikishikwa na Mkurugenzi wa benki ya CRDB,Abdulmajid Nsekela
Baadhi ya wafanyakazi walifurah Boss wao kuibuka kidedea kwani wanaamini mwakani katika Tuzo zinazofata ataibuka namba 1.

Karmali anaiongoza kampuni ya GF inayomiliki Kiwanda cha kuunganisha magari kilichopo Kibaha mkoani Pwani na pia ni wauzaji wa magari ya FAW,HONG YAN ambayo kwa sasa yanatengenezawa katika kiwanda kilichopo Kibaha mkoani Pwani pamoja na mitambo ya XCMG
Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar ,Omar Said Shaban(katikati) akimkabidhi Mkurugenzi wa kampuni ya GF Trucks & Equipment’s Ltd ,Imran Karmal tuzo ya CEO bora namba 2 wa mwaka 2022 wakati wa hafla ya tuzo za Tanzanite Top 100 CEO zilizofanyika jijini Dar es salaam.Kushoto ni mwenyekiti wa Tanzania Institute of Manager(TIM) Deogratius Kilawe.Picha na Said Khamis

Mkurugenzi wa kampuni ya GF Trucks & Equipment’s Ltd, Imran Karmal akizungumza wakati wa hafla kupokea tuzo hizo

3-Mkurugenzi wa GF akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa kampuni hiyo.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad