HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, October 15, 2022

NAIBU WAZIRI NDEJEMBI: MSITUMIE FEDHA ZA MKOPO KUOLEA MKE WA PILI, KUTUMBUA RAHA



Baadhi ya wananchi waliohudhuria uzinduzi huo.

 




Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Deo Ndejembi amewaasa wananchi kuacha tabia ya kutumia fedha za mkopo unaotokana na dhamana ya hatimiliki ardhi kuolea mke wa pili na kwenda mjini kutumbua raha.

"Mkitumia fedha hizo za mkopo zikaisha, taasisi za fedha mlikokopa zitakuja kutaifisha mashamba yenu,"Ndejembi.

Ndejembi ametoa onyo hilo alipokuwa akihutubia baada ya kuzindua jengo la masijala lililojengwa na Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) katika Kijiji cha Nakalonji, Kata ya Mbondo wilayani Nachingwea Oktoba 12, 2022.
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa MKURABITA, Mujungu Kasyenene akiwasalimia wananchi wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi.
PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA



Mdau, nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video, Naibu Waziri Ndejembi akiwaasa wananchi kuhusu matumizi ya mkopo...IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
MSIMAMIZI MKUU
KAMANDA WA MATUKIO TV/BLOG
0754264203

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad