HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, October 15, 2022

Meridianbet Wawafikia Wafanyabiashara Zaidi ya 300 Dar es Salaam!


SIKU ya kumbukizi ya Kifo cha aliyekuwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere Oktoba 14 ambayo hufanyika kila mwaka Mwaka huu Kampuni ya Meridianbet wameweza kutoa Aprons zaidi ya 300 kwa wafanyabiashara hasa baba lishe na mama lishe katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar- es salaam ikiwemo maeneo ya Makumbusho, Magomeni pamoja na eneno la Muhimbili.

Kama ilivyo kawaida ya Meridianbet, timu yao ikiongozwa na Afisa Masoko bwana Twaha Ibrahim, kampuni hii hutoa kile kidogo ambacho wanakipata na kukirudisha kwa jamii. Siku ya Nyerere Day, kampuni hii imeamua kuchagua kutoa Aprons kwa kina mama na baba ambazo zitawasaidia kwwenye uandaaji wa vyakula katika hali ya usafi.

Bila shaka kila mtu angependa kupata chakula magali safi, kilichoaandaliwa katika mazingira ya usafi. Meridianbet pia walitoa ujumbe huu kwa wafanyabiashara. Wakisisitiza kuwa wateja hawapendi kununua chakula au kula chakula ambacho hakijaandaliwa katika mazingira ya kuridhisha. Meridianbet wanajali jamii yake, wakiwemo wafanya biashara wenyewe.

"Tumekuja kuwashika mkono ndugu zetu wafanya biashara leo, tunawaoa Aprons ambazo zitawasaidia kuwaonesha kuwa hawa ni wafanya biashara wa chakula, lakini pia kuweza kuandaa chakula katika mazingira ya usafi. Aprons hizi zirawakumbusha kuwa sisi Meridianbet tunawajali, tuko pamoja nao" - Twaha Mohamed, Afisa Masoko

Katika maeneo ambayo wameweza kutembelea ikiwemo Makumbusho, wajasiriamali wa vyakula wamefurahi sana kwa kutembelewa na Meridianbet na kuletewa Aprons hizo huku wakisema zoezi hilo lisiishie hapo kwani uhitaji ni mkubwa sana kutokana na wingi wa wafanyabiashara.

"Tunashukuru kwa Aprons kutoka Meridianbet. Tunashukuru wametuona, tunaamini huu ni mwanzo wa mambo mengi mazuri. Sisi wafanyabiashaera tuna mahitaji mengi tu, na hili la Aprons uhitaji ni mkubwa sana. Tunashukuru Meridianbet" - Mama Aisha, Muza Chakula Makumbusho.

Meridianbet ni Kampuni bora na kongwe ya ubashiri Tanzania, ambayo imejipambanua kwa kutoa ofa bora za ubashiri wa michezo mingi, wakiwa na zaidi ya michezo 6000 ya kasino ya Meridianbet. Meridianbet pia hushirikiana na waandaaji wa michezo ya kasino kuendesha Jackpot za michezo ya kasino.

Jisajili na ubashiri na meridianbet kupitia www.meridianbet.co.tz, au piga *149*10# kubashiri bila intaneti ukiwa na mtandao wa Tigo na Airtel.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad