Mashirika
yasiyo ya kiserikali nchini yameagizwa kufungua akaunti zao katika
benki za nchini, na kwamba kwa kufanya kitendo hicho kimetajwa kama ni
sehemu ya uzalendo.
Wito huo ulitolewa na Waziri Mkuu, Mhe.
Kassim Majaliwa wakati akizungumza na wananchi na watumishi wa Benki ya
NMB alipotembelea banda la benki hiyo katika kilele cha Jukwaa la Mwaka
la mashirika yasiyo ya kiserikali.
Waziri Mkuu alitembelea NMB
kuanza mazungumzo na mashirika yasiyo ya kiserikali kote nchini ili
kuwafungulia akaunti ndani ya benki hiyo ambayo ina matawi 228 nchi
nzima na kusema mpango huo mbali na kuonyesha uzalendo, lakini itasaidia
kuongeza mzunguko wa fedha ndani ya nchi, jambo litakalotafsiriwa kama
kitendo cha kizalendo.
Meneja Mwandamizi wa Mahusiano wa benki
ya NMB, Bi. Dorah Monyo alisema utaratibu wa kuweka fedha kwa benki za
ndani utakuwa na faida kubwa kwa wananchi kwani mzunguko wa fedha
unabaki ndani na kumuahidi kuwa NMB itakuwa benki ya kwanza kusaidia
mashirika hayo kuwa na akaunti ndani ya benki na zenye uendeshaji wa
gharama nafuu.
Mwenyekiti wa Mtandao wa Mashirika yasiyokuwa ya
Kiserikali, Dk Lilian Badi alisema ni wakati kwa taasisi binafsi
kuwekeza fedha zao kwa mabenki ya nyumbani ili kuchangia ukuaji wa
uchumi.
Lakini pia, aliiomba Serikali kuzipa nafasi taasisi
zisizo za kiserikali ikiwemo kuwapa uhuru wa kufanya majukumu yao kwan
kwa sasa wamebanwa hasa kipengere cha usajili wa miaka 10 kwani
kinawakosesha nafasi ya kujadiliana na wadau kuhusu miradi mikubwa.
Waziri
Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa (kulia) akijadiliana jambo na wafanyakazi wa
Benki ya NMB alipotembelea banda hilo kwenye maonesho ya Jukwaa la
mwaka la Mashirika yasiyo ya Kiserikali lilolofanyika Jijini Dodoma.
Benki ya NMB ni mmoja wa wadau wa jukwaa hilo.
Meneja
Mwandamizi Mahusiano Benki ya NMB, Bi. Dorah Monyo (kushoto) akitoa
maelezo kwa Waziri Mkuu, Mhe. Kassim majaliwa (kulia) alipotembelea
banda hilo kwenye maonesho ya Jukwaa la mwaka la Mashirika yasiyo ya
Kiserikali – Dodoma.
No comments:
Post a Comment