Wafanyabiashara
wa Vinywaji pamoja na watumiaji wametakiwa kuwa na utaratibu wa
kuhakiki ubora wa vinywaji kabla ya kuvitumia kwa kutumia app maalumu ya
Hakiki stempu ili kutambua bidhaa feki ambazo zinaweza kuhatarisha afya
zao.
Wito
huo umetolewa hivi karibuni na Balozi Mradi wa Stempu za Kodi za
Kielektroniki (ETS) kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Ruekaza
Rwegoshora wakati akitoa elimu kwa wananchi waliotembelea maonesho ya
Nanenane yaliyofanyika kitaifa mkoani Mbeya wiki iliyopita.
Alisema
TRA inapenda kuwahamasisha wafanyabiashara na wananchi wanaotumia
bidhaa kama mvinyo wa zabibu, matunda aina mbalimbali, pombe kali, bia,
sigara na aina zingine za vileo kushiriki kulinda afya zao kwa
kuzihakiki kabla ya kuzitumia.
Rwegoshora
alisema App ya Hakiki stempu inauwezo wa kutambua uhalali wa bidhaa za
vinywaji ambazo zipo sokoni ambapo mtumiaji atapaswa kuwanayo katika
simu janja na kufanya uhakiki wa bidhaa iwapo inafaa kwa matumizi ya
binadamu.
"Hii
app maalumu ni bure na inapatikana katika hizi simu janja kazi yake ni
kuhakiki ubora wa vinywaji vyako, lengo la kuhakiki ubora wa bidhaa za
vinywaji ni kwa sababu kuna aina nyingi za bidhaa hizo siyo rahisi
kufahamu ubora wake," alisema
Amesisitiza
kuwa kwa kutumia mfumo huo wa app mfanyabiashara na mtumiaji ataweza
kupata taarifa sahihi kuhusu ilipotoka bidhaa,ilipotengenezwa,na lini
itaisha muda wake wa matumizi hivyo kumfanya mlaji wa bidhaa husika kuwa
salama.
Kwa
Upande wake balozi mwingine wa ETS kutoka TRA, Lewis Rwenyagira alisema
ETS ni alama maalum zinazobandikwa au kuchapishwa katika bidhaa ili
kuonyesha kuwa ni halalìna imezalishwa au kuingizwa nchini na
mfanyabiashara anayetambulika na amelipa kodi ya ushuru wa bidhaa
stahiki.
Hata
hivyo alisisitiza kuwa App hiyo ya kuhakiki bidhaa inafaida nyingi kwa
wafanyabiashara hasa pale wanapokwenda kununua vinywaji kwani
itawasaidia kutambua bidhaa feki pamoja na kufahamu ubora wake hivyo ili
kumlinda mteja.
Maofisa
wa Tra na mabalozi wa ETS wakitoa elimu wa wafanyabiashara wa vinywaji
waliotembelea viwanja vya nanenane jinsi ya kupakua na kutumia app ya
hakiki stempu kwa njia ya kielektroniki (ETS). Sikukuu za kitaifa za
maonesho ya nanenane zimefanyika jijini Mbeya wiki iliyopita kwa mwaka
huu wa 2022 na kuhudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mh. Samia Suluhu Hassan.
Ma
afisa mradi wa ETS kutoka TRA, Bw. Ruekaza Rwegoshora (L) Bw. Lewis
Rwenyagira,(C ) na balozi wa ETS/Hakiki stempu wakitoa ufafanuzi kwa
wanahabari (hawapo pichani) jinsi mfumo wa kielektroniki wa kuhakiki
stempu unavyofanya kazi katika viwanja vya maonesho ya kilimo Nanenane
yaliyofanyika kitaifa jijini Mbeya mwaka huu.
Ma
afisa mradi wa ETS kutoka TRA, Bw. Ruekaza Rwegoshora (L) Bw. Lewis
Rwenyagira,(C ) na balozi wa ETS/Hakiki stempu wakitoa ufafanuzi kwa
wanahabari (hawapo pichani) jinsi mfumo wa kielektroniki wa kuhakiki
stempu unavyofanya kazi katika viwanja vya maonesho ya kilimo Nanenane
yaliyofanyika kitaifa jijini Mbeya mwaka huu.
Balozi
wa ETS kutoka TRA akimsaidia mfanyabiashara kupakua app ya Hakiki
stempu kwa ajili ya kuhakiki ubora wa bidhaa, katika viwanja vya
maonesho ya kitaifa ya kilimo Nanenane jijini Mbeya.
No comments:
Post a Comment