Kabidhi Wasii Mkuu na Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Usajili, Ufilisi na
Udhamini (RITA,) Bi. Angela Anatory akizungumza katika kikao hicho
kilichowakutanisha na wadau wanaofanya nao kazi kwa ukaribu katika
utoaji huduma na kueleza kuwa majibu ya ufikiwaji wa usajili na utoaji
vyeti kwa watoto walio chini ya miaka mitano kwa asilimia 65 utatoa
majibu kupitia zoezi la sensa litakalofanyika Agosti 23 mwaka huu na
kuwataka watanzania kushiriki vyema zoezi hilo kwa manufaa na maendeleo
ya Taifa.
Msajili
wa matukio ya kijamii Zanzibar Mohamed Makame akizungumza wakati wa
kikao hicho na kueleza kuwa elimu kwa Umma inahitajika zaidi ili waweze
kuwafikia na kutoa huduma kwa wananchi wote ambao wanahitajika kutoa
taarifa sahihi na kupata haki ya kupata vyeti vyao vya kuzaliwa.
*
Mwamko mdogo wa watanzania kuandika Wosia waelezwa, watakiwa kuandika
na kuhifadhi Wosia kupitia RITA ili kuepusha migogoro ya kifamilia
WAKALA
wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA,) imepongezwa kwa jithada za
kufanikikisha usajili na kutoa vyeti kwa watoto walio chini ya miaka
mitano kwa asilimia 65 ukilinganisha na asilimia 13 ya zoezi hilo kwa
mwaka 2013.
Hayo yameelezwa leo na Katibu Mkuu wa Wizara ya
Katiba na Sheria Mary Makondo wakati akifungua mkutano ulioikutanisha
RITA na wadau wanaofanya nao kazi kwa karibu kikao kilicholenga kujadili
mafanikio, fursa kutoka kwa wadau katika kuboresha huduma pamoja na
hali ya ushirikiano na wadau pamoja na kutafuta suluhu za changamoto ili
kupanua wigo wa utoaji wa huduma.
Katibu Mkuu Makondo amesema,
ufanisi uliooneshwa na RITA katika kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa
kwa watoto walio chini ya miaka mitano katika mikoa 23 huku mikoa 3
iliyosalia kupatiwa huduma hiyo kwa siku za karibuni imelipa Taifa
heshima ya kutembea kifua mbele katika mkutano mkuu wa Mawaziri barani
Afrika utakaofanyika Oktoba mwaka huu ambapo kila nchi itaeleza hali ya
usajili na kwa Tanzania hali ni nzuri kutokana na ufanisi uliooneshwa na
RITA katika usajili wa na utoaji vyeti vya kuzaliwa kwa watoto walio
chini ya miaka mitano milioni 7.7 kwa msaada wa Serikali na wadau
mbalimbali wa maendeleo wakiwemo UNICEF, Balozi za Canada, Italy na
kampuni ya mawasiliano ya Tigo Tanzania.
Amesema, kikao hicho
kilichoikutanisha wakala hiyo na wadau wanaotumia huduma zao ni muhimu
katika kuboresha huduma za kijamii kupitia usajili huo ambao pia
husaidia Serikali katika mipango ya maendeleo pamoja na huduma za
kijamii ikiwemo afya na elimu.
'' Programu hii ya usajili na
kutoa vyeti kwa watoto walio chini ya miaka mitano iliyobuniwa na RITA
na kushirikiasha wadau wa maendele wakiwemo UNICEF ni muhimu sana na
imefanikiwa kwa kiwango kikubwa na fanisi wa hali ya juu..endeleeni
kutoa elimu kwa Umma juu ya umuhimu wa nyaraka hii muhimu na Wizara
inaielekeza RITA kuwa zoezi hili liwe endelevu ili kuwafikia watoto wote
nchini wakiwemo walio na miaka 7 hadi 18 ambao wapo katika mifumo rasmi
ya shule au vinginevyo kwa kuwa ni haki ya kila mtanzania kuwa na cheti
cha kuzaliwa.''Amesema.
Akieleza kuhusiana na mwamko wa
watanzania kuandika na kuhifadhi Wosia huduma ambayo inatolewa na RITA
Bi. Makondo amesema, mwamko si wakuridhisha hali inayosababisha
kuendelea kwa migogoro katika jamii huku waathirika wakubwa wakiwa ni
watoto na wanawake.
''RITA inaandika na kuhifadhi Wosia kwa
gharama nafuu kabisa na sio uchuro kufanya hivyo ni salama na uhakika
tukiwa hatupo kile tulichofanyia kazi kwa ajili ya familia zetu
kiendelee hivyo na tunachotakiwa kufanya ni kuandika wosia ili kuepusha
migogoro na kuweka salama familia na wapendwa wetu.'' Amesema.
Aidha
amesema kuwa Wizara imeielekeza RITA kufanya tafiti ya kwanini watu
wengi hawaandiki Wosia na dodoso litaweka katika tovuti ya wakala hiyo
na maoni yatakayotolewa na wananchi yatafanyiwa kazi katika kuboresha
kipengele hicho.
Pia amewataka wadau kuendelea kushirikiana
na Serikali ya Tanzania ambayo milango yake ipo wazi kwa ushirikiano
katika kuhakikisha jamii ya watanzania inafikiwa na huduma zote muhimu.
Kwa
upande wake Kabidhi Wasii Mkuu na Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Usajili,
Ufilisi na Udhamini (RITA,) Bi. Angela Anatory amesema, katika kuboresha
huduma kwa wananchi watakuwa wakikutana na wadau hao mara mbili kwa
mwaka ili kuboresha taasisi kwa manufaa ya jamii kwa kuhakikisha kupitia
TEHAMA wanafanikisha zoezi la usajili na utoaji vyeti vya kuzaliwa kwa
watoto walio chini ya miaka mitano na watanzania kwa ujumla kwa
ushirikiano wa karibu na wadau.
Amesema majibu ya ufikiwaji
wa watoto kwa asilimia 65 utaletwa na zoezi la sensa litakalofanyika
Agosti 23 mwaka huu na kuwataka watanzania kushiriki vyema zoezi hilo
kwa manufaa na maendeleo ya Taifa.
Kuhusiana
na mwamko wa watanzania kuandika na kuhifadhi Wosia kupitia RITA Bi.
Angela amesema bado ni mdogo na hadi sasa wakala hiyo imeandika na
kuhifadhi Wosia 700 na kutoa rai watanzania kutumia huduma hiyo ya
kuandika na kuhifadhi Wosia inayotolewa na wakala hiyo kwa gharama
nafuu.
Kikao hicho kilichobeba kauli mbiu ya 'Ushiriki wa Wadau
ni Muhimu katika Utoaji wa Huduma Bora, Kujenga Mifumo Thabiti, Kuongeza
Ubunifu na Kusogeza Huduma kwa Wananchi' kimeikutanisha RITA na wadau
mbalimbali zikiwemo benki, kampuni za mawasiliano, Balozi, taasisi za
Serikali na binafsi pamoja na viongozi wa dini ambao kwa pamoja wametoka
na maadhimio ya ushirikiano, matumizi ya TEHAMA pamoja na kutoa elimu
kwa juu ya umuhimu wa kuwa na nyaraka muhimu ya kuzaliwa na wametoa rai
kwa watanzania kushiriki zoezi la sensa litakalofanyika Agosti 23 ili
kuiwezesha Serikali kupanga mipango thabiti ya maendeleo na huduma za
kijamii. Baadhi
ya wadau wakitoa neno wakati wa kikao hicho ambapo wamehaidi
ushirikiano na Serikali kupitia RITA kwa manufaa ya watanzania.
Matukio mbalimbali katika picha wakati wa kikao hicho.
Matukio ya picha za pamoja za wadau walioshiriki katika kikao hicho.(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MASSAKA, MICHUZI TV.)
No comments:
Post a Comment