HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, June 1, 2022

TRA WAKABIDHI SHEHENA YA MBOLEA KWA JESHI LA MAGEREZA

 

 

Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) imeikabidhi Jeshi la Magereza kontena mbili za mbolea zenye thamani ya Shilingi Milioni 124 ambazo kimsingi umepitiliza muda wa forodha wa kuhifadhiwa  mahali hapo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi shehena hiyo yenye jumla ya mifuko 1960 ya mbolea hiyo aina ya YARA, Afisa Mfawidhi wa TRA katika Bandari Kavu ya 'Dar es Salaam Inland Container Depot' (DICD) Swalehe Rajabu alisema hatua hiyo ni utekelezaji wa mamlaka ya kisheria aliyopewa kamishna wa TRA.
Alisema baada ya mzigo huo wenye jumla ya Kontena tano kukaa kwa Musa mrefu mahali hapo, Kamishna Mkuu wa TRA Alphayo Kidata akaamuru mbolea hiyo kutolewa kwa taasisi mbalimbali zinazojihusisha na kilimo likiwemo Jeshi la Magereza.

" Huu ni utaratibu wa kawaida Kwa TRA pale inapotokea mzigo wowote kupitiliza muda wa kukaa kwa sheria na taratibu za kiforodha, tunaamini kwa kuwapatia magereza  mbolea hii kutawaongezea uzalishaji na hivyo kuleta tija kwa Taifa" alisema Rajabu
Akipokea msaada huo kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa Magereza nchini, Mkuu wa Magereza Dar es Salaam ACP George Wambuva mbali na kuishukuru TRA kwa msaada huo, alisema mbolea hiyo imekuja wakati muafaka ambao Jeshi hilo linajiandaa na msimu wa kilimo.

"Tunashukuru kwa msaada huu, ukweli sisi kama Jeshi la Magereza kilimo ni sehemu ya majukumu yetu hivyo imani yetu itatusaidia katika kufanikisha shughuli za kilimo na kukifanya kiwe na tija zaidi" alisema ACP Wambuva

Alisema malengo baadaa ya kuipokea mbolea hiyo wataipeleka katika Magereza ambazo shughuli za kilimo zinatekelezwa na kwamba kwa upande wao Dar es Salaam imekuwa kama sehemu ya kupokelea mzigo huo.

Aidha alisisitiza wanakwenda kuutumia  msaada huo kwa dhumuni lililokusudiwa kwa lengo la kuhakikisha wanaongeza tija katika uzalishaji wa mazao mbalimbali nchini 




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad