KuliaBw.
Raymond Mndolwa, akionesha sehemu ya daraja la mto Mvomero, halipo
katika picha, lililoharibiwa vibaya na athari zitokanazo na mabadiliko
ya Tabia nchi pamoja na shughuli za kibinadamu. wengine katika pichani
watumishi kutoka Halmashauri ya wilaya ya Mvomero na Ofisi za Tume ya
taifa ya Umwagiliaji Mkoani Morogoro.
Picha ikionesha sehemu za kingo za mto Mvomero zilivyoharibiwa vibaya na shughuli za binadamu.
Picha
ikimuonesha Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji akiwa na
wataalam katika kikao cha pamoja, kilichofanyika katika Ofisi ya
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mvomero kabla ya kwenda kutembelea Skimu ya
Kilimo cha Umwagiliaji Msufini.
Na Mwandishiwetu -Mvomero
MKURUGENZI
Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Raymond Mndolwa, amewaasa
wakulima nchini kutunza vyanzo vya maji kwa kutokufanya shughuli za
kibinadamu hususani za kilimondaniyamitasitini (60) ilikunusuru
kuharibika kwa kingo za mito unaopelekea uharibifu wa Miundombinu ya
kilimo cha Umwagiliaji.
Bw.Mndolwa
ameyasema hayo mapema alipokuwa akizungumza na wakulima wa skimu ya
Umwagiliaji Msufini iliyopo Wilayani Mvomero Mkoani Morogoro, inayotumia
maji kutoka mto Mvomero kama chanzo cha maji ya kilimo cha Umwagiliaji,
ambapo ameshuhudia uharibifu mkubwa uliofanyika kutokana na shughuli za
kilimo zisizorasmi.
Aliwashauri
viongozi wa S erikali yakijiji kushirikiana kulinda vyanzo hivyo vya
maji kwa manufaa ya kila mwananchi na aliendelea kusema “Hatulindi
vyanzo vya maji yakunywatuu, hata vya kilimo na kuzuia uharibifu
unaofanywa na binadamu wenzetu, asili inaharibiwa na
binadamu.”Alisisitiza
Bw.
Mndolwa aliagiza wataalam kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji
nawataalam kutoka Halmashauri kufanya mapitio ya mto na chanzo nakuona
athari iliyotokana na mafuriko yaliyopita katika mto huu.
Katika
zoezi hilo wataalam watatakiwa kuja na mapendekezo yanini kifanyike ili
kurekebisha athari za mafuriko hali itakayopelekea skimu ya Msufini
kuanza kufanya kazi.
Aliongeza
kuwa, kitachofanyika kwa sasa nikutengeneza chanzo kinachopeleka maji
katika skimu hiyo matengenezo ambayo yataridhisha pande zote ikiwa ni
pamoja na serikali na watumiaji wa skimu hiyo.
“siwezi
ruhusu mkandarasi aliyefanya kazi kwa kiwango cha chini upande mwingine
aje tena hapa,sababu kuna mahali kaharibu na nitamfukuza, kama kaharibu
kwingine na hapa ataharibu.”Alibainisha Mndolwa.
Kwa
upande wake Kaimu Mkurugenzi Idara ya Miundo mbinu kutoka Tume ya Taifa
ya Umwagiliaji, Mhandisi Ntonda Kimasa alisema, kuwa mradi huo
umetengewa fedha kwa mwaka wafedha 2022/2023 kwa ajili yakuboresha
miundombinu yake, hivyo mara baada ya kukamilika mapendekezo ya timu
kazi ya ukarabatiwa miundombinu itaanza mara moja.
Awali,
Bw. Mndolwa aliwakumbusha wakulima swala zima za kulipa Tozo na ada za
matunzo ya skimu za Umwagiliaji baada ya kujengewa na kukarabatiwa kwa
miundombinu hiyo.
Kwa
upande mwingine aliwashauri wadau husika akitolea mfano wadau wa
barabara, kilimo na wadau wengine wakae kwa pamoja ili yafanyike
maamuzi sahihi na kuona namna ya kuunusuru mto mvomero kutokuacha njia
yake ya asili na kupelekea kuvamia makazi ya watu.
Skimu
ya kilimo cha Umwagiliaji Msufini, iliyopo Wilayani Mvomero Mkoani
Morogoro pamoja na kuathiriwa na athari zitokanazo na mabadiliko ya
Tabia nchi,imeharibiwa vibaya nashughuli za kibinadamu zinazofanyika
ndani ya mita sitini, bila kuzingatia sheria.
No comments:
Post a Comment