NA. MWANDISHI WETU
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na
Uratibu Mhe. George Simbachawene amekabidhi rasmi mradi wa ujenzi wa
Kituo cha Usimamizi wa Maafa kilichopo eneo la Nzuguni “B” Jijini Dodoma
kwa mkandarasi Lwanda Limited kutoka Morogoro.
Akizungumza
wakati wa hafla hiyo iliyofanyika tarehe 14 Mei, 2022 na kuhudhuriwa na
viongozi wa ofisi yake pamoja mshauri elekezi na mkandarasi amewataka
kukamilisha mradi huo kwa wakati kwa kuzingatia umuhimu wa kituo hicho
katika kuratibu shughuli za maafa nchini.
Aliongezea kuwa,
tayari fedha zimeshatolewa kiasi cha shilingi bilioni 2.442 ambazo
zitatumika kuhakikisha ujenzi unaanza haraka bila kukwama.
“Kipekee
nimpongeze Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kutoa fedha
kuhakikisha ujenzi unaanza ili kuendelea kuratibu masuala ya maafa kwa
ufanishi mkubwa hivyo ipo haja ya kuifanya kazi hii kwa weledi na
kuikamilisha kwa wakati,”
Uwepo wa kituo utasaidia kuongeza hali
ya usalama katika anga, nchi kavu na kwenye maji kwa kuzingatia
jitihada za serikali katika kuhakikisha usalama wa wananchi ili
kuendelea kushiriki katika shughuli za kimaendeleo kwa utulivu.
Akitoa
taarifa ya mradi huo Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi
ya Waziri Mkuu Meja Jenerali Michael Mumanga alisema mradi umetengewa
eneo la ukubwa wa ekari 106 hivyo kituo kinatarajiwa kuwa kikubwa
chenye kukidhi mahitaji yaliyopo nchini ili kutoa huduma kwa viwango
vinavyotakiwa.
“Muda wa utekelezaji wa mradi ni miezi 12 baada
ya makabidhiano ya eneo la kazi na kazi zitaanza rasmi tarehe 30 Mei,
2022 na tunatarajia mkandarasi aukabidhi mradi huu tarehe 29 Mei,
2023,”alieleza Meja Jenerali Mumanga
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. George Simbachawene akikata utepe ikiwa ni ishara ya kukabidhi rasmi mradi wa ujenzi wa Kituo cha Usimamizi wa Maafa kwa mkandarasi wa LADWA limited tarehe 14 Mei, 2022 Nzuguni ‘B’ Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. George Simbachawene akikabidhi nyaraka kwa mkandarasi kutoka LADWA limited wakati wa hafla ya kukabidhi mradi wa Kituo cha Usimamizi wa Maafa nchini kitakachojengwa katika eneo la Nzuguni ‘B’ Jijini Dodoma.Halfa hiyo ilifanyika tarehe 14 Mei, 2022.
No comments:
Post a Comment