Na Mwandishi wetu, Mirerani
Wanawake
wafanyakazi wa Tume ya Madini Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani
Manyara, katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani, wamesherehekea
siku hiyo na watoto yatima na wenye kuishi kwenye mazingira magumu
wamekabidhi vyakula katika kituo cha Light In Africa, Mirerani.
Mfanyakazi
wa Tume ya Madini Mirerani, Zainab Athuman amesema wamewakabidhi watoto
hao vyakula mbalimbali ikiwemo mchele, soda, sabuni, mafuta na kula nao
keki.
Zainab amesema
wameshiriki siku hiyo kwa kuwatembelea watoto hao, kuwapa vyakula na
kula keki pamoja katika kuwathamini watoto hao.
"Wafanyakazi
wote wa Tume ya Madini Mirerani tumeshiriki kuchanga fedha zetu na
kununua zawadi hizi za watoto hawa yatima na wenye kuishi kwenye
mazingira hatarishi," alisema.
Mmoja kati ya watoto hao, Caroline Zacharia amewashukuru wanawake hao kwa kuwapatia msaada huo.
Caroline amesema watu wanapowatembelea na kuwapatia msaada hujisikia faraja na kuona wanapendwa na jamii inayowazunguka.
Mwenyekiti
wa bodi ya Light In Africa, Vincent Mamasita amewasihi wadau wengine
waige mfano huo katika kuwachangia watoto wenye uhitaji.
Mamasita amesema katika kituo hicho cha Light In Africa Mirerani wanawahudumia na wamewagawa watoto wakiume, wakike na walemavu.
No comments:
Post a Comment