Shirika
lisilo la kiserikali, T-MARC Tanzania ambayo ni mshirika wa karibu wa
serikali katika mapambano ya vita dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi
imedhihirisha umahiri wake katika maonyesho ya wiki moja ya siku ya
Ukimwi duniani yaliyohitimishwa Jana katika Uwanja wa Ruandansovwe,
jijini Mbeya.
Kwa
mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari ilitotolewa na T-MARCK ilisema
kuwa maonyesho hayo yalihitimishwa kwa kusherehekea siku ya Ukimwi
duniani ambayo kitaifa ikifanyika jijini hapa.
T-MARC
Tanzania ilishiriki kwa kuwa na banda kwenye wiki ya maadhimisho hayo
ambayo kwa mwaka huu yana kauli mbiu inayosema “Zingatia Usawa.Tokomeza
Ukimwi. Tokomeza Magonjwa ya Mlipuko” kutokana na kuwa mshirika wa
karibu wa serikali ya Tanzania katika vita vya mapambano dhidi ya
Ukimwi.
Katika
maonyesho hayo banda la T-MARC lilionekana kuwa kivutio kutokana na
namna ambavyo walionyesha umahiri katika shuguli zake za huduma za afya
ikiwemo mapambano dhidi ya Virusi vya Ukimwi, Kifua Kikuu, uzazi wa
mpango, afya ya uzazi, lishe, Malaria, Maji na suala la usafi wa
mazingira pamoja na kuhamasisha utoaji wa nafasi kwa mtoto wa kike
katika maendeleo yake.
Katika
elimu waliyokuwa wakitoa T-MARC wameweza kueleza bayana kuhusu njia
inayotumiwa zaidi kupata maambukizi ya Ukimwi kutoka kwa mtu mmoja
kwenda kwa mwingine ni ya kujamiana ambayo huchangia kwa asilimia 80.
Katika
week hii ya maonesho T-MARC imepeleka mafunzo ya kuhamasisha matumizi
ya Kondom zao pendwa za Dume Classic, Dume Desire, na Dume Extreme,
ambazo zinalenga rika mbalimbali na watu wenye kipato tofautitofauti
huku wakilenga vijana na watu walio kwenye sehemu hatarishi.
Hadi sasa T-MARC imeuza na kuzambaza kondom milioni 60 katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.
Ikiwa
kama kitovu cha utendaji uliotukuka, T-MARC Tanzania ina Jukumu ya
kuhakikisha jamii inapata huduma za afya za kudumu na za uhakika kwa
kushirikiana na washirika wake, na imekuwa ikifanya hivyo katika miaka
inayokaribia 20.
No comments:
Post a Comment