Bodi
ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imefanya kongamano la 12 la
Mwaka lililowakutanisha wataalam zaidi ya 1200 ikiwa na lengo la
kujadili ubunifu wenye suluhisho katika utekelezaji wa Ununuzi na Ugavi
kwa kutambua ushindani na mapinduzi ya Viwanda kwa maendeleo ya Jamii.
Kongamano hilo lililoanza Novemba 30 hadi Desemba 03 mwaka 2021.
Akizungumza
wakati wa kufunga Kongamono hilo Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI,
Profesa Riziki Shemdoe aliyemwakilisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Ummy Mwalimu amesema
wakurugenzi wa mamkala za Serikali za Mitaa kuhakikisha wanafuata
ushauri wa Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi ili kuepusha upatikanaji wa
hati chafu kwenye Mamlaka hizo hasa kwenye taasisi zote za Serikali.
Amesisitiza
kuwa taaluma waliyoisomea iweniya kuleta tija na ufanisi kwenye Miradi
ya Serikali hivyo Wataalam hao wanapaswa kuwa na weledi na pia ambao
wanaheshimu taaluma yao.
Shemdoe
amesema kuna waajiri ambao wanaajiri maafisa Ununuzi na Ugavi ambao
hawajasajiliwa na Bodi kuwa wahakikishe wafanyakazi wao wawe
wamesajiliwa na Bodi ya PSPTB ili kusaidia pale wanapokutana Wataalam
hao kujadiliana masuala yao kwa uhuru na uwazi.
Amezitaka
taasisi zote zilizoko chini ya Mamlaka ya Serikali ya Mitaa na
zilizochini ya wizara ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI kuhakikisha wataalamu
wote ambao wameajiriwa lakini hawajasajiliwa na Bodi ya PSPTB
wanasajiliwa haraka kulingana na Sheria iliyoianzisha PSPTB
inavyoelekeza.
Katibu
Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe akizungumza na
Wataalam wa Ununuzi na Ugavi pamoja na wafanyakazi wa Bodi hiyo kuhusu
namna walivyojipanga kuwasimamia na kuisimamia taaluma hiyo ili kuwa na
tija kwenye maendeleo ya Taifa wakati wa kufunga Kongamano la 12
Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi lililokuwa na kauli mbiu ya kujadili
ubunifu wenye suluhisho katika utekelezaji wa Ununuzi na Ugavi kwa
kutambua ushindani na mapinduzi ya Viwanda kwa maendeleo ya Jamii.
Kongamano hilo lililoanza Novemba 30 hadi Desemba 03 mwaka 2021.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB) Godfred Mbanyi
akizungumza wakati na Wataalam wa Ununuzi na Ugavi pamoja na
kumkaribisha mgeni rasmi Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Profesa
Riziki Shemdoe aliyemwakilisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za
Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Ummy Mwalimu kwa ajili ya kufunga
Kongamano la 12 la mwaka la Wataalam wa Ununuzi na Ugavi.
Baadhi
ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi wakifuatilia mada kwenye Kongamamo la
12 la wataalam hao lililoanza Novemba 30 hadi Desemba 03 mwaka 2021
likiwa na kauli mbiu ya kujadili ubunifu wenye suluhisho katika
utekelezaji wa Ununuzi na Ugavi kwa kutambua ushindani na mapinduzi ya
Viwanda kwa maendeleo ya Jamii.
Meneja
Masoko na Uhusiano kwa Umma ( PSPTB), Shamim Mdee akizungumza jambo
kwenye kongamano la 12 la mwaka la Wataalam wa Ununuzi na Ugavi
Katibu
Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe akiwa kwenye picha
ya pamoja na makundi mbalimbali mara baada ya kufunga Kongamano la 12 la
Mwaka la Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi lililofanyika jijini Arusha.
No comments:
Post a Comment