MFUKO
wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umetwaa Tuzo ya
Umahiri katika Uwasilishaji wa Taarifa za mahesabu kwa mwaka 2020.
Akizungumza
baada ya kupokea Tuzo hiyo katika hafla ya kufunga mafunzo pamoja na
utoaji wa Tuzo za umahiri katika uandaaji wa Taarifa za Fedha ya Mwaka
2020 (Best Presented Financial Statements for the Year 2020 Awards) kwa
Taasisi, Makampuni pamoja na Mashirika zinazotolewa na Bodi ya Taifa ya
Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) zilizofanyika katika
hotel ya APC Bunju jijini Dar es Salaam Desemba 4, 2021, Mkurugenzi wa
Fedha, PSSSF, Bi. Beatrice Musa-Lupi alisema Ushindi huo ni ishara ya
kwamba PSSSF inaandaa mahesabu kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa
kimataifa lakini pia inaashiria uwepo wa weledi wa tasnia husika kwa
upande wa watumishi.
“Sambamba
na hayo niliyoyasema pia inaashiria uwepo wa usimamizi makini wa fedha
za wanchama na hii inatupatia heshima kama taasisi.” Alisema Mkurugenzi
huyo wa Fedha PSSSF.
Aliwahakikishia
Wanachama dhamira ya PSSSF kuhakikisha usalama wa michango yao
unazingatiwa kwa kiwango cha juu wakati wote, ikiwa ni pamoja na kuwepo
uwazi kwenye usimamizi na utunzaji wa rasilimali za Mfuko.
“Ushindi
huu pia unaashiria uwepo wa kesho ya wanachama wetu kama kaulimbiu yetu
inavyosema Leo. Kesho. Pamoja.” Alihitimiaha Bi. Beatrice Musa-Lupi
Mkurugenzi
wa Fedha, PSSSF, Bi. Beatrice Musa-Lupi (kulia) akipokea tuzo hiyo
kutoka kwa mgeni rasmi, Mhasibu Mkuu wa Serikali Bw. Leonard Mkude.
Washindi
wa Kwanza wa tuzo zilizotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi
wa Hesabu Tanzania (NBAA) wakiwa katika picha ya pamoja na meza kuu
Mkurugenzi wa Fedha, PSSSF, Bi. Beatrice Musa-Lupi (kulia) na Bi. Grace Kabyemela, Mhasibu Mkuu wa PSSSF wakionyesha tuzo hiyo.
No comments:
Post a Comment