HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, December 7, 2021

MZUNGUKO WA SITA HATUA YA MAKUNDI YA LIGI YA MABINGWA KUMALIZIKA WIKI HII

*Maliza Mzunguko Kibingwa Kwa Kubashiri Na Meridianbet Wiki Hii!

BAADHI ya timu zimeshafuzu hatua ya Mtoano kunako Ligi ya Mabingwa, zingine, bado zinajitafuta na michezo ya mwisho itaamua. Wiki hii mambo yapo hivi;

AC Milan kuwaalika Liverpool pale San Siro katika mtanange wa kuhitimisha hatua ya makundi kwenye Uefa Champions League. Liverpool ameshafuzu hatua ya mtoano, Milan anahitaji ushindi ili kujihakikishia walau anacheza Europa msimu huu. Itawezekana? Meridianbet tumekuwekea Odds ya 2.18 kwa Milan.

 

Kule Amsterdam, Uholanzi, Ajax watachuana na miamba ya soka la Ureno - Sporting CP. Vijana wa Erik Ten Hag, wameshafuzu hatua ya mtoano, watoto wa Lisbon wanatafuta uhakika wa kufuzu. Kupoteza mchezo wa awali ni kumbukumbu waliyonayo Sporting, itawapa motisha au watadidimia? Odds ya 1.48 imewekwa kwa Ajax kupitia Meridianbet.

 

Mbivu na mbichi zitakuwa pale Allianz Arena. FC Bayern Munichen uso kwa uso na FC Barcelona. Huu ni msimu ambao, pengine tutawaona Barca wakicheza Europa au kuwa nje ya mashindano ya Ulaya. Kimsingi, ili Barca wafuzu hatua ya mtoano kwenye Ligi ya Mabingwa, wanahitaji ushindi dhidi ya Bayern ambao tayar wameshafuzu lakini, wapo moto! Odds ya 1.67 imewekwa kwa Bayern.

 

Kwenye kundi F, nani ataungana na Manchester United kwenye hatua ya mtoano? Atalanta kuchuana na Villarreal jumatano hii. Mshindi kati yao, atafanikiwa kutinga hatua ya mtoano huku aliyepoteza akichukua uelekeo wa Ligi ya Europa. Nani ni nani? Ifuate Odds ya 1.76 kwa Atalanta wiki hii.

 

Alhamisi, macho na masikio yatakuwa pale Maradona Stadium, Napoli vs Leicester City. Timu mbili ambazo zimetoka kupokea vichapo kwenye ligi zao. Kwenye msimamo wa kundi lao, kinara (Leicester) anachuana na anayemfuata kwa karibu (Napoli). Dakika 90 kuweka sawa msimamo wa Kundi C. Meridianbet tumekuwekea Odds ya 2.08 kwa Napoli.

Meridianbet – Nyumba Yenye Odds Bora na Bonasi Kubwa!

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad