Uogozi
wa Shirika la Childbirth Survival International(CSI) wakiwa kwenye
picha ya pamoja na walimu wa Chuo cha Urembo Maznat pamoja na washiriki
waliofika kwenye usaili wa kuwapata vijana wawili uliofanywa chini ya
CSI na Chuo cha Urembo cha Maznat .
Na Said Mwishehe, Michuzi TV
SHIRIKA
la Childbirth Survival International(CSI) tangu kuanzisha kwake miaka
10 iliyopita limefanya mambo makubwa hasa katika eneo la kupunguza vifo
vya mama mjazimto na watoto chini ya miaka mitano.
Aliyekuwa
Balozi wa Tanzania nchini Marekani ambaye kwa sasa ni Waziri wa Mambo
ya nje na ushirikiano wa kimataifa wa Tanzania, Balozi Liberata
Mulamula(kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mwanzilishi wa Shirika la Childbirth Survival International(CSI)Tausi Hamis Kagasheki(kulia) alipokuwa ametembelea banda la Shirika ilo nchini Marekani
Hata
hivyo kwa mwaka huu wa 2021 limefanya mambo mbalimbali katika jamii ya
Watanzania na moja ya kazi hizo ni uamuzi wake wa kuwa na programu
maalum ya kuwasaidia vijana kiuchumi kwa kufanikisha ndoto zao.
Kupitia
programu hiyo CSI ilijikita katika kuwatafuta vijana wenye ndoto na
kisha kuzifanikisha.Hivyo ilibeba jukumu, kwanza la kuwatafuta vijana
wenye ndoto kupitia kongamano maalumu lililofanyika Mombasa jijini Dar
es Salaam, na baada ya hapo vijana waliopatikana walipatiwa nafasi ya
kupelekwa Chuo cha Urembo Maznat na kulipia gharama zote, kuanzia ada ya
masomo hadi nauli za usafiri wa kwenda na kurudi kwa muda wote wa
masomo.
Madakatari
kutoka hospitali mbalimbali za Jijini Dar es Salaam wakiendelea na kazi
ya kuwachunguza watoto Njiti kwa ajili a kujua afya zao ili kuwaepusha
na magonjwa mbalimbali yanayoweza kuwakabili wakati wa zoezi la kutoa
huduma za kiafya kwa watoto njiti iliyoandaliwa na Dorris Mollel
Foundation na kufanyika katika ukumbi wa Don Bosco jijini Dar es Salaam.
Ukweli
programu hiyo ya CSI kwa mwaka 2021 imebadilisha maisha ya vijana
wengi, hata wale ambao hawakubahatika kuchaguliwa, kuanzia hapo
walibadili mitazamo yao na kuona kumbe wanaweza kutimiza ndoto zao kwa
kufanya shughuli za kuwapatia kipato.
Hivyo
wakati mwaka 2021 unakwenda kumalizika, vijana wanabakia na kumbukumbu
nzuri namna CSI ilivyowashika mkono kwa vitendo, iliona haja ya kuwabeba
na kufanikisha ndoto zao.
Baadhi
ya vijana waliobahatika kupata nafasi ya kufadhiliwa masomo na CSI
wamesema 2021 unabakia kuwa mwaka wa kumbukumbu kubwa katika maisha yao
itakayochukua miaka mingi kufutika.
Kwa
kukumbusha tu programu ya kuwasaidia vijana ilianza Januari mwaka 2021
na katika kongamano la kuwatafuta vijana kwa ajili ya kuwasaidia
walijitokeza zaidi ya 100 na kati ya hao wawili wakabahatika kupata
ufadhili wa masomo.
CSI
imefanya hivyo kwa kuamini vijana ndio wazazi wa kesho , na
wakiwezeshwa kiuchumi itakuwa rahisi kumudu kuhudumia familia zao, hivyo
kupunguza changamoto za kimaisha zikiwemo za kumudu gharama za matibabu
ya afya hasa kupunguza vifo kwa mama mjawazito na mtoto.
David
Francis ambaye aliibuka mshindi kwenye usaili wa kuwapata vijana wawili
uliofanywa chini ya CSI na Chuo cha Urembo Maznat akizungumza na
waandishi wa habari kuhusu namna alivyojiamini mpaka kuwa mshindi kwenye
shundano hilo.
David
Francis Matongo ni mmoja ya wanufaika wa mradi wa kusaidia vijana ,
hivyo anasema mwaka 2021 kwake umekuwa wenye bahati kubwa , ndio mwaka
uliomkutanisha na CSI inayoongozwa na kusimamiwa na wamama wawili wema
wenye nia ya kusaidia wengine.
"Nikiri
mwaka 2021 umenikutanisha na CSI, umenikutanisha na watu wema ambao kwa
kweli wamebadilisha maisha yangu. Ndoto yangu ya muda mrefu ilikuwa ni
kujifunza urembo , nashukuru CSI wameifanya itimie katika mwaka
huu,"amesema.
Meneja
wa Programu za Vijana katika shirika la Childbirth Survival
International(CSI) Ester Mpanda pamoja na wanafunzi wakipata maelekezo
kutoka kwa uongozi wa Chuo cha Urembo Maznat mara baaada ya kuwasili
chuoni hapo kwa ajili ya kuanza masomo ya urembo
Anaeleza
anakumbuka Januari 2021 CSI walitafuta vijana."Tulikuwa wengi siku ile
na mimi nikabahatika, Februari 19 nilianza masomo Chuo cha Urembo
Maznat, tuligharamiwa kila kitu na CSI."
David
anasema CSI imenisaidia kutimiza ndoto zake na sasa anaweza kumudu
maisha yake, kupitia ujuzi ambao ameupata amekuwa akifanya shughuli zake
na kumuingia kipato."Mwaka 2021 kwangu unabakia kuwa mwaka
mzuri,ahsanteni CSI kwa wema wenu huu."
Wakati
anazungumza na Michuzi Blog na Michuzi TV katika mwaka huu, David
ameweka wazi ambavyo sasa anaweza kupamba bibi harusi, kupamba majukwaa,
kutengeneza kucha, kufanya masaji , kusuka na kufanyia mtu make Up.Yote
hayo amejifunza kwa ufadhili wa fedha za CSI.
Meneja
wa Programu za Vijana katika shirika la Childbirth Survival
International(CSI) Ester Mpanda akizungumza na washiriki wakati wa
mchakato wa kuwapata vijana hao kupitia usaili uliofanywa chini ya CSI
na Chuo cha Urembo Maznat ili kuwapata vijana wawili watakaofadhiliwa na
shitika hilo kwenye masomo ya urembo.
Kwa
upande wake Meneja Programu za Vijana wa CSI Ester Mpanda wakati
anazungumza siku walipozindua programu hiyo alieleza wazi CSI wanaamini
unapomuandaa kijana wa leo katika kutimiza ndoto yake kimaisha, maaa
yake unamsaidia kiuchumi.
Madakatari
kutoka hospitali mbalimbali za Jijini Dar es Salaam wakiendelea na kazi
ya kuwachunguza watoto Njiti kwa ajili a kujua afya zao ili kuwaepusha
na magonjwa mbalimbali yanayoweza kuwakabili wakati wa zoezi la kutoa
huduma za kiafya kwa watoto njiti iliyoandaliwa na Dorris Mollel
Foundation na kufanyika katika ukumbi wa Don Bosco jijini Dar es Salaam.
"Kwa
muda wote CSI tunaendelea kutimiza majukumu yetu kwa kushirikiana na
Serikali, kwetu sisi tunajisikia fahari kuona takwimu zinaonesha vifo
vya mama mjamzito na watoto chini ya miaka mitano vikiendelea
kupungua.Pamoja na hayo tumeona haja ya kuwasaidia vijana kupitia
programu hii."
Kuhusu
CSI, ni shirika la kimataifa ambalo limeanzishwa na wamama wa wawili
Tausi Hamis Kagasheki anayeishi nchini Marekani ambako ndiko yalipo
makao makuu ya CSI pamoja na Mama Stella Mpanda anayeishi nchini
Tanzania.
Wamama
hao jasiri waliamua kuanzisha shirika hilo ikiwa ni mkakati wa
kukabiliana au kupunguza vifo kwa mama mjazito na mtoto wakati wa
kujifungua.Ukweli wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa.Kwa kutambua thamani
ya uhai waliamua kupanua wigo, hivyo CSI , na zaidi wamekuwa
wakitekeleza majukumu yao katika nchi nyngine .
Meneja
wa Programu za Vijana kutoka CSI, Ester Mpanda, timu ya Shirika la
Childbirth Survival International(CSI) pamoja na timu ya Dorris Mollel
Foundation wakiwafanyia usajili mama na mtoto waliofika kwa ajili ya
watoto Njiti kufanyiwa uchunguzi na madaktari kutoka hospitali ya
Muhimbili, Aga Khan na kuandaliwa na Dorris Mollel Foundation
iliyofanyika Don Bosco jijini Dar es Salaam
Kupitia
CSI wamekuwa wakitoa elimu kwa jamii kuhusu kutambua afya ya uzazi
salama kupitia programu mbalimbali ambazo wamekuwa wakizitoa kwa zaidi
ya miaka 10 sasa sambamba na kusaidia vifaa vya kujifungulia katika
hospitali mbalimbali nchini.
Mbali
ya Tanzania, CSI ipo pia katika nchi za Somalia, Rwanda, Uganda,
Marekani, na wanarajia kuwa na tawi nchini Burundi pamoja na Kenya kwa
nchi za Afrika Mashariki.
Meneja
wa Programu za Vijana Shirika la Childbirth Survival International(CSI)
CSI, Ester Mpanda akizungumza kuhusu CSI Tanzania inavyoshirikiana na
Doris Mollel Foundation wakati wa maadhimisho Siku ya Mtoto Njiti
Duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo Novemba 17 ya kila mwaka
yaliyofanyika katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam
No comments:
Post a Comment