HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, December 24, 2021

Airtel yazindua ‘Tabasamu na Airtel TUNAKUJALI’ maalum kusaidia jamii

 


Tabasamu na Airtel TUNAKUJALI’ Kunufaisha mikoa 12
 

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania kupitia mpango wake wa Airtel TUNAKUJALI leo imetangaza kuzindua kampeni maalum ili kuendeleza jitihada zake za kusaidia jamii kwa kipindi hiki cha msimu wa sikukuu ambayo inalenga kuwanufaisha watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu. Kampeni hiyo itajulikana kama ‘Tabasamu na Airtel TUNAKUJALI’, kupitia kampeni hiyo itanufaisha mikoa 12 kwa kugusa vituo 12 vinavyolelea watoto nchini ili kuwapa tabasamu kwa kipindi hiki cha sikukuu za Krismas na Mwaka

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa kutangaza kuzindua kampeini hiyo ya ‘Tabasamu na Airtel TUNAKUJALI’, Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano alisema, “katika msimu huu wa sikukuu tendo hili ni moja ya njia yetu ya kuonyesha upendo kwa watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, tumewiwa kuwafanya watabasamu, kuwaonesha tunawajali na kuwapa matumaini ya baadae, kwa msimu huu wa sikukuu tunawapa hiki kidogo kwa upendo ili na wao waweze kusherehekea sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya. Tutaoa msaada kwenye vituo 12 vya watoto vilivyopo katika mikoa ya Rukwa, Katavi, Kigoma, Lindi, Kagera, Mtwara, Singida, Dodoma, Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya.

Singano aliongeza, “Furaha ya Airtel siku zote imekuwa ni kuwa sababu ya kubadilisha maisha ya wengine kupitia miradi mbali mbali kama Airtel TUNAKUJALI Tunaamini katika dhana ya jamii iliyo sawa na ndio sababu tumechangua msimu huu wa sikukuu kuishi na hawa watoto”.

Singano aliongeza kuwa kwa muda mrefu, Airtel Tanzania imekuwa ikifanya miradi mbali mbali ya kusaidia jamii kwenye afya na elimu. Mradi wetu wa Airtel Tunakujali ulizinduliwa mnamo 2014 kwa kwa kuwashirikisha wafanyakazi wa Airtel kuwa na utamaduni wa kusaidia jamii yetu na wamefanya hivyo. Airtel TUNAKUJALI imekuwa ni chachu kubwa katika kutuunganisha sisi Airtel na jamii. Sisi Airtel tunaendelea kusaidia jamii inayotuzunguka kama moja ya njia ya mafanikio yetu, Singano alisema.

Vituo hivyo 12 kila moja itapata zawadi ya Krismas na Mwaka Mpya ya Tzs 2 milioni.

Kwa uapande wake Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mheshimiwa Godwin Gondwe ambaye alizindua kampeni hiyo ya ‘Tabasamu na Airtel TUNAKUJALI’ aliwashukuru Airtel kwa kusaidia watoto hasa hasa kwa kuwakumbuka wanaoishi kwenye mazingira magumu kwa kipindi hiki cha msimu wa sikukuu.

‘’Natambua kuwa kampuni ya Airtel Tanzania inamilikiwa na serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia 49 na nina uhakika chini ya umiliki mpya, Airtel itaendelea sio kuwekeza tu kwenye masuala ya kusaidia jamii lakini pia upanuzi wa mtandao kitu ambacho ni lazima tukipongeze’, Gongwe alisema.

Nimepewa taarifa kuwa Airtel Tanzania kwenye kusaidia jamii imeshirikiana na serekali kwenye ujenzi wa Hospitali ya Uhuru jijini Dodoma kwa kutoa zaidi ya shilingi bilioni 2. Ujenzi wa hospitali hiyo unaendelea na ukikamilika itakuwa ni moja ya hospitali kubwa, yakisasa kwenye ukanda huo. Bado naendelea kushuhudia Airtel ikiendelea kurudisha kwa kusaidia jamii mnayoihudumia, leo hii nashuhudia ‘Tabasamu na Airtel TUNAKUJALI’ ambayo imekuja wakati muafaka ambapo marafiki na wanafamilia wakisherehekea na watoto wetu hawa watasherehekea pia. Nawapongeza sana na nawaomba muendelee kusaidia jamii na hasa watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, Gondwe aliongeza.

Nae mmoja kati ya wa kituo cha watoto wanaoishi kwenye changamoto cha Sinza Ijango ambao ni kati ya wafaidika wa kampeini ya "Tabasamu na Airtel’ TUNAKUJALI, Latifa Mahmoud alisema kuwa ni muhimu jamii itambue na kupongeza juhudi kubwa zinazofanywa na makampuni binafsi kama Airtel ya kusaidia jamii ambayo inaishi kwenye mazingira magumu.

Aliongeza, “Msaada wenu umekuja kwenye muda muafaka kwani sisi watoto tanaoishi kwenye vituo hivi wanahitaji kusherehekea kama wengine. Kwa kweli tunashukuru sana na tunaomba muendelee na moyo huo huo wa kuasaidia wengine.







Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Godwin Gondwe (kulia) akimkabidhi Mwakilishi wa Kituo Cha Yatima cha Sinza Ijango cha jijini Dar es Salaam baadhi ya msaada uliotelewa na kampuni ya Airtel Tanzania kwa vituo 12 vya watoto yatima ikiwa ni ishara ya kuonyesha upendo kwa kipindi hiki cha msimu wa sikukuu. Airtel Tanzania kupitia mpango wake wa Airtel TUNAKUJALI leo imetangaza kuzindua kampeni maalum ili kuendeleza jitihada zake za kusaidia jamii kwa kipindi hiki cha msimu wa sikukuu ambayo inalenga kuwanufaisha watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu. Kampeni hiyo itajulikana kama ‘Tabasamu na Airtel TUNAKUJALI’. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad