MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma, (PSSSF) umetoa wito kwa Wanachama na Wananchi kwa ujumla kuchangamkia fursa ya huduma ya kuwawezesha kumiliki nyumba kwa kulipa kidogokidogo na hivyo kuboresha maisha yao.
Wito
huo umetolewa na Mkurugenzi wa Fedha wa Mfuko huo, Beatrice Musa-Lupi
aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wakati wa ufunguzi rasmi wa
Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini
Dar es Salaam Novemba 10, 2021 ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Waziri wa
Nchi Ofisi ya Rais, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (Anayeshughulikia
masuala ya Fedha na Mipango) Mhe. Jamal Kassim.
Akifafanua
kuhusu umiliki huo Lupi alisema PSSSF na Benki ya Azania wanayo
makubaliano yanayowawezesha wananchama na wananchi kukopa kutoka benki
hiyo kupitia mikopo ya makazi yaani (Mortgage loan) ili kununua nyumba
na viwanja vinavyomilikiwa na PSSSF kama vile nyumba za makazi za Buyuni
jijini Dar es Salaam.
“Tunashirikiana
na wenzetu wa benki ya Azania, mwanachama na asiye mwanachama
anakaribishwa kwenye banda letu hapa Mnazi Mmoja atakutana na maafisa wa
Mfuko ambao wako tayari kutoa huduma na kuwapa elimu kuhusu majukumu ya
Mfuko lakini pia elimu ya fedha kuhusu jinsi Mwanachama au Mwananchi
atakavyoweza kununua nyumba hizo kupitia mkopo kutoka benki ya Azania
kwa masharti nafuu.” Alifafanua Mkurugenzi huyo wa fedha wa PSSSF.
Kama ambavyo kauli mbiu ya Wiki hiyo inavyosema “Boresha Maisha Kupitia Elimu ya Fedha, PSSSF ni miongoni mwa taasisi za fedha iliyo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu ikiwa na jukumu la Hifadhi ya Jamii.
“Hifadhi
ya Jamii ina majukumu mengi ikiwemo Kusajili Wanachama, Kukusanya
Michango, Kuwekeza kwa mujibu wa Sheria lakini pia kulipa Mafao
mbalimbali kwa Wanachama na kwa kupitia uwekezaji tunaamini elimu
tunayoitoa hapa itawawezesha wanachama na wanachi kutambua fursa
zilizopo na hivyo kuboresha maisha yao binafsi na hivyo kuchangia pato
la taifa.” Alisema
No comments:
Post a Comment