Na Mwandishi wetu
IMEELEZWA
kuwa Katika kuwajengea uelewa wananchi, Serikali kupitia Wizara ya
Madini imeandaa semina elekezi juu ya uanzishwaji wa Vituo vya Mfano vya
Katente na Lwamgasa pamoja na miradi mipya ya uchimbaji mkubwa wa
madini kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini.
Lengo
ni kuwa chachu ya kuwahabarisha wabunge wengine na baadaye wabunge
kutoa elimu hiyo kwa wananchi ili kama nchi kuwa na uelewa juu ya
masuala mtambuka yanayosimamiwa na Wizara ya Madini.
Hayo
yalibainishwa na Waziri wa Madini, Doto Biteko alipokuwa akizungumza na
wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini na viongozi wengine wa
Wizara waliohudhuria semina hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Wizara
ofisi ndogo zilizopo GST mjini Dodoma.
Alisema
ujenzi wa vituo hivyo uliwezeshwa kwa fedha kutoka Benki ya Dunia
ujenzi wa vituo vya mfano vilivyojengwa ili kuwasaidia wachimbaji wadogo
kutoka katika uchimbaji duni na kuchimba kwa teknolojia rahisi na bora
ili waweze kuchimba kwa tija pia semina hiyo imegusia eneo la leseni ya
uchimbaji mkubwa ya Tembo Nickel Corporation iliyotolewa hivi karibuni
ili kuwafahaisha wabunge matarajio ya uchimbaji huo pamoja na changamoto
zinazoambatana nayo.
Alisema
kufuatia maelekezo yanayotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania ya kuifungua sekta ili watu wengi zaidi waweze kushiriki katika
kuwekeza kwenye Sekta ya Madini. Waziri Biteko alisema hivi sasa
Serikali inakwenda kutoa leseni tatu (3) za uchimbaji mkubwa wa madini
ambazo hazijatolewa kwa miaka 15 iliyopita ikiwa ni pamoja na kufufua
miradi iliyokuwa imesimama kwa muda mrefu kama ule wa Buckreef kuanza
uzalishaji.
Aidha,Waziri
Biteko aliwashukuru wajumbe wa Kamati hiyo kwa michango na maelekezo
yao na kuahidi kufanyia kazi maelekezo na maoni waliyotoa yenye lengo
la kuifanya Sekta ya Madini kujiendesha kwa tija.
Akiwasilisha
mada juu ya uanzishwaji wa vituo vya mfano vya Katente na Lwamgasa
Mhandisi Moses Kongola alisema vituo hivyo vilianzishwa kwa lengo la
kuwawezesha wachimbaji kuchimba kwa kutumia teknolojia sahihi na ya
kati yenye urahisi katika kuitumia huku ikihusisha gharama nafuu.
Alibainisha
kuwa uanzishwaji wa vituo hivyo utawasaidia wachimbaji wadogo kuongeza
uzalishaji wa madini na mapato, kupata maarifa na ujuzi, utahamasisha
afya na usalama migodini pamoja na kupunguza athari za kijamii na
mazingira wakati wa shughuli za uchimbaji na uchenjuaji wa madini.
Kwa
upande wake, Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Yahya
Samamba akiwasilisha mada juu ya miradi ya uchimbaji mkubwa wa madini
alisema ili mradi ujulikane kama ni uchimbaji mkubwa lazima uhusishe
umiliki wa leseni ya uchimbaji mkubwa wa madini ambayo uwekezaji wake
unaanzia Dola za Marekani milioni 100.
Aidha,
mhandisi Samamba alibainisha kuwa mradi wa uchimbaji Mkubwa wa Madini
ya Nickel unamilikiwa na Kampuni ya Tembo Nickel Corporation Limited
(TNCL) kwa ubia kati ya kampuni ya Kabanga Nickel Limited (KNL) ya
nchini Uingereza na Serikali ya Tanzania kupitia Msajili wa Serikali.
Alisema
utekelezaji wa mradi huo utafanyika katika eneo la Kabanga wilaya ya
Ngara mkoani Kagera ambapo uhai wa mgodi huo ni miaka 33 utakao iletea
serikali mapato ya kiasi cha dola za Marekani 7,543,065,250 sawa na
shilingi za kitanzania trilioni 17.35 kwa kipindi chote cha uzalishaji.
Makamu
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini na Mbunge
wa Jimbo la Manonga, Seif Gulamali alizungumza kwa niaba ya wajumbe wa
kamati hiyo aliitaka Wizara ya Madini kuhakikisa inashughulikia vibali
vyote vitakavyohitajika na kampuni ya Tembo Nickel Corporation Limited
kwa ajili ya kuendelea na utekelezaji wa mradi huo ili kusiwe na mkwamo
wowote na hivyo kupelekea mradi kukamilika na kuanza uzalishaji kwa
wakati.
Akitoa
maelekezo juu ya usimamizi wa Vituo vya Mfano vilivyojengwa kwa fedha
zilizotolewa na Benki ya Dunia vya Katente na Lwamgasa, Gulamali
aliagiza miradi hiyo iwe na matokeo chanya kwa maana ya kuwa na faida
kwa taifa na faida kwa wananchi wanaonufaika na miradi hiyo ili
uwekezaji uliofanywa katika maeneo hayo uwe na tija.
Kwa
upande wake, Mbunge wa Ngara, Ndaisaba George alisema wananchi wa Jimbo
la Ngara, kata na vijiji vinavyozunguka mradi huo wameupokea vizuri
mradi wa uchimbaji wa madini ya nickel na wapo tayari kufuata maelekezo
ya serikali ili waweze kupisha mradi mara baada ya fidia kulipwa na
kupewa maeneo watakayopaswa kuhamia.
Alibainisha
kuwa, kiasi cha dola za Marekani milioni 59 zimetengwa kwa ajili ya
kulipa fidia wananchi wa eneo hilo wanaotarajia kuachia maeneo yao mara
tu ya fedha hizo kulipwa kwa wananchi na kuwezesha mradi kuendelea
pasipokuwa na migogoro yeyote wakati wa utekelezaji wake.
Mafuzo
kama haya yanalenga kuongeza uelewa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Nishati na Madini inayoisimamia Wizara ya Madini juu ya kazi
zinazotekelezwa na wizara na kuwaongezea wajumbe wa kamati uwanja mpana
wa uelewa juu ya miradi inayosimamiwa na wizara.
No comments:
Post a Comment