Waziri
wa Mifugo na Uvuvi – Mashimba Ndaki (kushoto) akishuhudia uwekaji saini
ya makubaliano kati ya NMB na kampuni ya Bima ya Britam juu ya kutoa
Bima kwa Wavuvi na Vyombo vyao maarufu kama Jahazi. Wanaotia Saini ni
Afisa Mkuu wa wateja Binafsi na Biashara Filbert Mponzi(wa pili kulia)
na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Britam Raymond Komanga (tai
nyekundu) katika hafla iliyofanyika jijini Mwanza jana. Kulia ni Mkuu
wa Idara ya Bima NMB – Martin Massawe
Afisa
Mkuu wa wateja Binafsi na Biashara Filbert Mponzi(wa pili kulia) na
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Britam Raymond Komanga(tai
nyekundu) wakionesha kwa waandishi wa habari mikataba muda mfupi baada
ya utiani sasa rasmi na kuzindua Bima ya Wavuvi na Vyombo vyao, katika
hafla ya utiaji Saini iliyofanyika jijini Mwanza jana mbele ya waziri wa
Waziri wa Mifugo na Uvuvi – Mashimba Ndaki(kushoto), anayeshuhudia ni
Mkuu wa Idara ya Bima wa NMB Martin Massawe(kulia).
Afisa
Mkuu wa wateja Binafsi na Biashara Filbert Mponzi(wa pili kulia) na
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Britam Raymond Komanga(tai
nyekundu) wakibadilishana mikataba, muda mfupi baada ya utiani sasa
rasmi na kuzindua Bima ya Wavuvi na Vyombo vyao, katika hafla ya utiaji
Saini iliyofanyika jijini Mwanza jana mbele ya waziri wa Waziri wa
Mifugo na Uvuvi – Mashimba Ndaki(kushoto), anayeshuhudia ni Mkuu wa
Idara ya Bima wa NMB Martin Massawe(kulia).
Afisa
Mkuu wa wateja Binafsi na Biashara Filbert Mponzi(wa pili kulia) akitoa
maelezo ya kuhusu bima ya Jahazi kwa Waziri wa Kilimo na Uvuvi Mashimba
Ndaki(wa tatu kushoto) wakati wa uzinduzi wa Bima hiyo uliofanyika
jijini Mwanza Mbele ya Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Britam
Raymond Komanga(kushoto), Katibu Tawala wa Wilaya ya Nyamagana Alfred
Yonas (wa pili kulia), na Afisa Mkuu wa Rasilimali watu wa NMB –
Emmanuel Akonaay(kulia)
……………………………………………………………..
Na Mwandushi wetu – Mwanza
BENKI
ya NMB kwa kushirikiana na kampuni ya Bima ya Britam wamezindua bima
maalum ijulikanayo kama Jahazi kwa ajili ya kuwasaidia wavuvi katika
mikoa mbalimbali hapa nchini.
Bima
hiyo ilizinduliwa jana jijini Mwanza na Waziri wa Mifugo na Uvuvi,
Mashimba Ndaki inalenga kutoa nafasi kwa wavuvi kupata kinga wanapopata
majanga mbalimbali.
Akizungumza
katika uzinduzi huo, Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB –
Filbert Mponzi, aliserma bima hiyo inawalenga wavuvi wadogo na wa kati
hapa nchini.
Alisema
wavuvi watakata bima ya asimilia 3 ya chombo husika cha shughuli ya
uvuvi na kwamba wataweza kukingwa na majanga ya ajali, kuungua mitumbwi
ama boti pamoja na watu watakaokuwa ndani ya vyombo hivyo.
Aliongeza
kuwa faida nyingine za bima hiyo ni pamoja na familia ya mvuvi ama mtu
aliyekuwa ndani ya chombo hicho kupewa mkono wa pole endapo kutatokea
kifo pamoja na kupata ulemavu wa kudumu.
Aidha,
bima hiyo itatoa gharama za matibabu kwa mvuvi pamoja na kulipwa fidia
kutokana na ajali yoyote itakayompata atakapokuwa majini kwa ajili ya
shughuli za uvuvi ama kando kando ya ziwa, mto, bwawa ama bahari.
Mponzi
aliwataka wavuvi kufika katika ofisi za NMB kwa ajili ya kukata bima
ambayo itawakinga na majanga mbalimbali wanapokuwa katika shughuli zao
kwenye maziwa, mito, mabwawa na bahari.
Akizungumza
katika uzinduzi huo, Meneja wa kampuni ya Bima ya Britam kanda ya ziwa,
Said Kadabi alisema kwamba bima hiyo itawasaidia wavuvi katika kuinuka
kiuchumi kwa kuwa sasa watanya kazi zao kwa kujiamini.
Alisema
wanalenga kuyafikia makundi mbalimbali ya kijamii na kuyakatia bima
ikiwamo mama lishe ili waweze kufanya shughuli zao kwa kujiamini zaidi.
Kwa
upande wake, Waziri Ndaki aliwataka wavuvi kutumia fursa hiyo kukata
bima ili iwasaidie kuwakinga wanapokumbwa na majanga mbalimbali.
Alisema
siku za nyuma bima ilikuwa inawaangalia wavuvi wakubwa pekee na kwamba
kwa sasa NMB na Britam wamekuja na aina mpya ya kuwasaidia wavuvi wadogo
na wa kati.
Aliwataka
wavuvi waendelee kupewa elimu ya bima ili waijue na kufanya maamuzi kwa
kuwa ni njia sahihi ya kuwasaidia katika kipindi chote wanapokuwa
katika shughuli zao.
Alisema
NMB imedhamiria kuwainua kiuchumi wakulima, wafugaji na sasa ni zamu ya
wavuvi na kwamba serikali inatambua mchango wao katika kuhakikisha
makundi hayo yananufaika na mikopo inayotolewa na benki hiyo.
Alisema
sekta ambazo zilikuwa zinaonekana kuwa na ‘risk’ kwa sasa zianze
kufikiwa na kukatiwa bima kwa kuwa zina mchango mkubwa katika uchumi wa
nchi.
Waziri
Ndaki alisema sekta ya uvuvi inaajiri watu milioni 4.5 na kwamba
inachangia asilimia 1.7 ya pato la taifa hivyo ni kundi muhimu ambalo
linatakiwa kusaidiwa ili liweze kupiga hatua.
No comments:
Post a Comment