Na WAMJW, Dodoma.
Serikali
kupitia Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
imemtambua Mwanariadha Michael Filberth Nondo, mkazi wa Kigoma
aliyejitolea kutembea kutoka mkoani Kigoma mpaka mkoani Kilimanjaro kwa
lengo la kuelimisha na kuhamasisha wananchi kuhusu ugonjwa wa UVIKO-19
na kuchanja Chanjo dhidi ya Uviko -19.
Katibu Mkuu Wizara ya ya
Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Prof. Abel Makubi,
ameueleza Umma kupitia Vyombo vya Habari akimwakilisha Waziri wa Afya,
Dkt. Dorothy Gwajima jijini Dodoma.
“Kama Serikali tunatambua
juhudi zinazofanywa na wadau mbali mbali katika Mapambano haya ya
Corona, lakini kwa leo kama Wizara niseme, tumetambua ndugu Michael
Nondo, aliye onesha Ujasiri na Uzalendo wakutembea kutoka mkoani Kigoma
mpaka mkoani Kilimanjaro ikiwa ni sehemu yakuunga Mkono juhudi zinazo
endelea nchini kote.” Amesema Prof. Makubi.
Kwa kutambua Mchango
wake, Prof. Makubi amemkabidhi Cheti na kumpa hadhi ya ukamanda wa
Kuhamasisha Wananchi kupata Chanjo kwa kuthamini mchango na uzalendo
wake katika kampeni hiyo ya uchanjaji.
Kwa upande wake,
mwanariadha huyo amesema, sababu kubwa iliyo msukuma kufanya zoezi hilo
ni imani aliyonayo juu ya serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
na sekta zote ikiwemo sekta ya Afya katika Mapambano dhidi ya Uviko- 19.
Hii
ni mara ya pili kwa Nondo, kufanya safari hiyo baada ya kufanya zoezi
kama hilo mwezi wa sita Mwaka huu kwa mara ya kwanza, kisha kujipumzisha
kwa miezi miwili kabla ya kurudia tena awamu hii,
“Mara ya
kwanza kufanya safari hii nilikuwa nikifanya usiku lakini hivi sasa
nimeamua kufanya mchana ili kila mmoja anione, ninawashukuru sana
Serikali hususan ngazi za Serikali za mitaa nilipoweza kupita ambapo
walinipa sehemu za kulala na kunikutanisha na wananchi, kunitambulisha
na kuongea nao kwa lengo la kutoa Elimu juu ya ugonjwa huu” amesema
Nondo
Ametoa wito kwa vijana, watu wa makamo na wazee kwenda
kupata chanjo kwa hiari kwa sababu chanjo hiyo haina madhara na kushauri
kuacha kusikiliza tetesi zisizokuwa za kweli na zenye lengo la
kupotosha.
Amewataka watanzania wajue kuwa Taifa linawahitaji
kwaajili ya kujenga Taifa hivyo kujitokeza kupata Chanjo pamoja na
kuchukua tahadhari za Maradhi ikiwepo UVIKO-19 ni muhimu sana kwao.
No comments:
Post a Comment