Kundi maalum kwa watumiaji wa huduma hizo litawapatia watumiaji wake kuwasiliana, kuuliza maswali mbalimbali yanayohusu bidhaa hizo na kujibiwa, ikiwa ni sehemu ya kuwaleta pamoja na kuwarahisishia kupata huduma kwa haraka.
Akizungumza katika hafla fupi ya kuzingua kundi hilo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya iStore Tanzania, Vipul Shah alisema kuwa kuzinduliwa kwa Kundi hilo kutasaidia kuwaleta pamoja wameteja wao na kuwarahisishia kupata huduma kwa haraka.
“Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita kumekuwa na ongezeko kubwa la matumizi ya bidhaa za Apple nchini Tanzania hasa simu za iPhone, hivyo kuanzishwa kwa kundi hili kutasaidia kuwaleta pamoja watumiaji wote na wateja wetu kwa ujumla ili kupata huduma kwa harama” alisema Shah.
Aliendelea kusema kuwa “Hivyo nawaasa wale wote ambao sio watumiaji wa huduma zetu waanze sasa kwani kuna kuna faida kubwa sana ukiwa mtumiaji wa bidhaa za Apple”.
Mratibu wa Usambazaji wa Kampuni ya Redington, Vipul Prajapati (kulia) akimkabidhi tuzo maalum kutoka Kampuni ya Apple, Meneja Uendeshaji wa Kampuni ya iStore Tanzania, Jully Martin katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ofisi za iStore, Mikocheni jijini Dar es salaam hivi karibuni. Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya iStore Tanzania, Vipul Shah.
No comments:
Post a Comment