WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso ametembelea mradi wa maji Mharamba katika jimbo la Geita vijijini na kuridhishwa na maboresho yaliyofanyika na kupelekea vituo vilivyokuwa havitoi maji kuanza kutoa huduma.
Waziri
Aweso ametoa maagizo kuwa vituo 3 vilivyobakia vianze kutoa huduma
katika kipindi cha wiki mbili ikiwa ni pamoja na kufanya upanuzi wa
mradi huu mkubwa pamoja na kuwaunganishia wananchi majumbani. Mradi huu
una jumla ya vituo 20 na kwa sasa jumla ya vituo 17 vinatoa huduma
kutoka katika tanki la lita 135,000.
Aidha Mh.Aweso amezitaka
kamati za maji vijijini kuweka utaratibu mzuri wa matumizi na ukusanyaji
wa fedha kutokana na uwepo wa baadhi ya kamati kuvuja fedha
zinazokusanywa kwenye miradi.
Aweso ameyasema hayo wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi Wilayani #Geita kwenye kijiji cha Mwaramba,Kata ya #Nkome.
Kufatia uwepo wa taarifa kutokuwa sahihi ya kamati ya Maji kijiji cha Mwaramba kwenye suala la makusanyo.
Kufatia
Hali hiyo Mkuu wa wilaya ya Geita, ambaye pia ni kaimu Mkuu wa Mkoa wa
Geita, #Wilson Shimo ameliagiza Jeshi la Polisi na Takukuru kuwakamata
na kufatilia uchunguzi wa mradi huo.
No comments:
Post a Comment