HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, August 13, 2021

MSIMU MPYA, VIBE JIPYA NDANI YA EPL NA LALIGA WIKIENDI HII

  *Burudika na Msimu Mpya wa Soka Ukiwa na Familia ya Meridianbet!

BAADA ya kukaa miezi 3 bila soka la vilabu barani Ulaya, hatimaye Agosti 13,2021 imefika na viwanja vyote kuanza kurindima kwa takribani miezi 8 ya msimu mpya wa soka 2021/22. VAR, vyenga vya kila aina, vita vya maneno ndani na nje ya uwanja – zote ni burudani za soka. Hakika, msimu mpya, vibe jipya! Tunaanza msimu mpya kwa namna hii;


Ijumaa hii, EPL itaukata utepe wa msimu mpya wa Ligi Soka nchini Uingereza kwa mchezo wa Brentford FC dhidi ya Arsenal. Wageni wa EPL – Brentford wataitupa karata yao ya kwanza dhidi ya vijana wa Mikel Arteta ambao hawatokua na michezo ya mashindano ya Ulaya baada ya kufanya vibaya msimu uliopita. Hii ni fursa ya timu hizi kuanza msimu huu kwa alama 3 muhimu kuelekea michezo 38 ya kukamilisha msimu. Meridianbet tumekuwekea Odds ya 1.95 kwa Arsenal.


Jumamosi kutachezwa mchezo wa mahasimu wa soka kwenye historia ya soka la Uingereza. Hapa ni Manchester United vs Leeds United ndani ya Old Trafford! Msimu uliopita, United alianza kwa kupoteza mchezo akiwa nyumbani. Lakini Leeds United alikula 6-2 alipocheza dhidi ya United pale Old Trafford, msimu huu itakuaje? Timu zote zimefanya usajili wa kutosha lakini dakika 90 zitaamua nyota ya nani itang’ara mbele ya mashabiki. Meridianbet tumekuwekea Odds Bora ya 1.54 kwa The Red Devils.


Pale Goodison Park, Rafael Benitez ataitupa karata yake ya kwanza akiwa kocha wa Everton kwenye mchezo dhidi ya Southampton. Benitez anakibarua cha ziada msimu huu, kuipata Imani ya mashabiki wa Everton ambao wengi wao wamepinga uamuzi wa klabu hiyo kumpatia mikoba ya Carlo Ancelotti. Ataweza kuwaonesha kuwa yeye ni mtu sahihi wa kuiongoza Everton licha ya kuwa aliwahi kuwa kocha wa Liverpool ambao ni mahasimu wakubwa wa The Toffees? Ifuate Odds ya 2.00 kwa Everton ukiwa na Meridianbet.


Macho ya wadau wengi wa soka la LaLiga na mashabiki wa FC Barcelona yatakua pale Nou Camp Jumapili hii. Barca watawaalika Real Sociedad kwenye mchezo wao kwanza bila Lionel Messi. Baada ya miaka 21, Messi ameondoka Nou Camp na sasa anapatikana kule Paris akiwa na Neymar Jr na Kylian Mbappe ndani ya PSG. Safari ya Barca bila nyota wao na nyota wa dunia yatakuaje? Mdhamini shujaa wako kupitia Meridianbet kwa kuifuata Odds ya 1.80 kwa Barcelona.


Wiki itaanza kwa mchezo wa Elche vs Athetic Bilbao kunako LaLiga Sentander. Msimu uliopita, timu zote zilikuwa zikidemadema kuokoa nafasi zao kwenye msimamo wa Liga hiyo, msimu huu wataanzaje na pengine watamaliza vipi? Mchongo upo Meridianbet, Odds ya 2.15 kwa Bilbao ipo kwa ajili yako.


Meridianbet, Nyumba Yenye Odds Bora na Bonasi Kubwa!


2 comments:

Post Bottom Ad