Na Mwandishi wetu
Mwaka
huu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan katika
Ikulu ya Magogoni Dar es Salaam aliwaapisha rasmi mabalozi wateule 13
kati ya 23 aliowateua Mei mwaka huu.
Miongoni
mwa mabalozi wateule walioapishwa ni Hoyce Anderson Temu anayekwenda
kuhudumu kama Naibu Mkuu wa kituo Jiji la Geneva, nchini Uswizi.
Balozi
Hoyce Temu anayetoka kwenye kada ya uandishi wa habari na ulimbwende
ana uzoefu wa miaka zaidi 15 katika masuala ya mawasiliano na mahusiano
ya umma akiwa amefanya kazi katika taasisi nyingi yakiwamo Mashirika ya
Umoja wa Mataifa (UN) na Benki.
Balozi
Hoyce Temu akiwa katika mashirika ya Umoja wa Mataifa alifanyakazi kwa
ufanisi mkubwa na kuweza kuyaweka mashirika hayo mbele ya wananchi wa
Tanzania na serikali akiwa kama mwamvuli kwa Serikali na Umoja huo kwa
kukuza mahusiano ya mashirika zaidi ya 23 yalipo chini ya UN.
Kwa
kutumia taaluma yake ya mawasiliano aliwezesha agenda za UN za
Maendeleo Endelevu (SDGs) kueleweka miongoni mwa Watanzania na hivyo
kushirikisha katika mipango mbalimbali ya maendeleo. Kwa kutumia elimu
yake ya diplomasia na habari alikuwa msambazaji mkuu wa agenda hizo.
Balozi Hoyce Temu katika shughuli zake za mahusiano amekuwa chachu ya kuunganisha Umoja wa Mataifa na Mabalozi wa mbalimbali kupata misaada ya kimaendeleo ndani ya nchi ikiwa ni tofauti kabisa na miaka iliyopita ya kwamba fedha nyingi zilikuwa zikitumwa moja kwa moja kutoka makao makuu kuja serikali ya Tanzania kama msaada wa UN ambapo kupitia uchangishaji huo (fund raising) ulifanikishwa na Jumuiya ya Umoja wa nchi za Ulaya (EU), Uswidi, Finland na nchini nyingine kupata fedha za ndani na kuwezesha makundi mbalimbali kutambua fursa na kuzitumia.
Uteuzi
wa Rais Samia Suluhu Hassan kwa nafasi hiyo na hata maelezo yake
kwanini ameteua watu chini ya miaka 45 na kuangalia utumishi wao katika
maeneo mengi yakiwemo waliofanya na mashirika ya UN inaonesha dhahiri
kuaminika kwa Balozi Hoyce katika ufanyaji wake kazi.
Pamoja
na mashirika ya UN wakati wa ulimbwende alionesha ubunifu wa hali ya
juu kwa kuendesha mambo ambayo awali hayakuwapo katika Miss Tanzania
hapo awali. Kuanzia kipindi chao walitembelea mikoa yote ya Tanzania
akatengeneza harambee za kutafuta fedha kwa ajili ya wahitaji.
Ikumbukwe
kuwa Balozi Hoyce Temu alipata taji la urembo wa Tanzania mwaka 1999 na
kuiwakilisha nchi katika mashindano ya mrembo wa dunia nchini
Uingereza.
Akiwa
mlimbwende mwaka 1999 pia aliajiriwa na Shirika la Chakula na Kilimo
(FAO) kama Afisa Uhusiano kwa miaka mitatu wakati huo Matron na Patron
wa mradi wa Telefood ya FAO ya kukusanya chakula na kusaidia makundi
mbalimbali ambapo Matroni na Patroni walikuwa Hayati Rais mstaafu
Benjamini Mkapa na Mama Anna Mkapa walisafiri mikoa yote ya nchi
kuwafikia makundi ya wanawake mbalimbali kuendesha miradi ya maziwa,
mashine na kufuga kuku ambapo wanawake wengi waliondolewa katika
umaskini uliokithiri kupita mradi huo huku Balozi Hoyce akiwa kama
sektretari wa kamati ya Telefood.
Balozi
Hoyce alikuja na wazo la mpango wa chakula kwa kikapu (Baskets for
Food) ikiwa moja ya kazi yake wakati wa taji lake na kuwafikia wanawake
wa Singida ambapo vikapu vilivyosukwa na wanawake hao vilipelekwa
Marekani vikauzwa katika makanisa na magulio mbalimbali nchini humo na
fedha kurejeshwa nchini na hivyo kusaidia familia nyingi kuwa na uwezo
wa kifedha na kusaidia kaya zao huku vikundi vya akina mama vikiwezeshwa
kimtaji na kuwa na uwezo wa kiuchumi.
Mwaka 2011 Hoyce alianzisha kipindi cha kusaidia wahitaji wa Tanzania ambao walihitaji fedha na faraja katika maisha yao.
Kazi
za utangazaji wa kipindi cha runinga cha "Mimi na Tanzania" ambacho kwa
sasa kinaitwa "Tanzania Yetu" ilimnadi binti huyu kama mwanamke
anayejali na kudhihirisha kwamba urembo alioufanya ulikuwa urembo wenye
nia na wenye malengo, kusaidia umma.
Kwa mujibu wa takwimu mtandaoni hadi Machi 2016 kipindi hicho kimesaidia watu 1,000 kwenye maeneo mbalimbali nchini.
Ukiangalia
mambo mengi ambayo Balozi Hoyce Temu amefanya nchini kusaidia
watanzania unabaini kwamba binti huyu ni tunda halisi la Kitanzania
lililoiva katika anga ya Kidiplomasia na mahusiano ya umma.
Kwa
uzoefu wa miaka 15 katika Diplomasia, Balozi Hoyce Temu bila shaka
anaenda kufanya vyema kwenye majukumu yake hayo mapya pamoja na kuwa
chachu ya kuitambulisha Tanzania duniani akiendeleza kasi yake
aliyofanya akiwa katika Mashirika ya Umoja wa Mataifa wakati
akifanyakazi nao kutoka hapa nchini.
Ifahamike
kazi kubwa ya Ubalozi wa Tanzania mjini Geneva ni kuhakikisha kwamba
inaendeleza mahusiano mazuri na Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya
kimataifa yaliyopo Geneva na Vienna Austria.
Pamoja
na kuwezesha Tanzania kujulikana pia kama alivyoagiza Rais Samia katika
hotuba yake ya kuwaapisha watakuwa na kazi kubwa ya kuhudumia
watanzania wanaoishi Uswizi wakiwemo dayaspora na wakazi wa Uswizi ambao
wanataka kuja nchini Tanzania katika masuala mbalimbali ikiwemo Utalii,
Uwekezaji na masuala mengine ya Kidiplomasia.
Katika
hotuba yake Julai 27 mwaka huu, mambo mengine ambayo Rais alisisitiza
na mabalozi vijana kutumia uwezo wa vijana katika dunia yenye mabadiliko
mengi kusimamia ushindani katika masuala ya uchumi ambayo sasa yapo
kitehama zaidi.
Julai
27 Mabalozi hao wanaoenda vituoni wametakiwa kusimamia Utalii, kulinda
rasilimali, kukuza uhusiano na mahusiano ya kiuchumi, 'digital
revolution', kuwezesha utalii wa tiba, na mengine mengi na kutokana na
uzoefu wake na elimu yake bila shaka Balozi Hoyce Temu atawakilisha
ufanisi na kasi kubwa kutokana na umri wake.
Kwa
mujibu wa kitabu cha 'Nayakumbuka Yote' cha Balozi Hoyce Temu cha mwaka
2007, ukurasa wa kwanza wa kitabu hicho inaeleza kuwa alizaliwa
Hospitali ya Mount Meru Mkoa wa Arusha, Machi 20 ,1978.
Alipata
elimu yake ya awali na Msingi Mkoani Moshi katika shule ya msingi
Matemboni Old Moshi ambako alisoma mpaka darasa la sita na kuhamishiwa
shule ya Arusha ambako alifanya mtihani na kufaulu kuingia shule ya
sekondari Arusha na shule kidato cha sita na tano kusomea shule ya
Wasichana ya Zanaki Jijini ya Jijini Dar es Salaam.
Alipata Digrii yake ya kwanza kutoka Chuo Kikuu cha Arizona State cha nchini Marekani.
Baada
ya kumaliza shahada ya kwanza alifanya kazi kama Meneja mahusiano na
mawasiliano katika Benki ya Standard Chartered na kisha kuchukua Post
graduate diploma katika Chuo cha Diplomasia, Dar es salaam.
Baada
ya kumaliza alijiunga katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine na
kuchukua Digrii ya Mawasiliano ya Umma na sasa yupo mwaka wa 4 katika
masomo ya PHD ya mawasiliano Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine.
Kuna
tuzo nyingi zimekwenda kwa Balozi Hoyce kabla ya uteuzi wake kuwa
balozi. Miongoni mwa tuzo hizo ni ya Uhuru wa Vyombo vya Habari
iliyotolewa na UNESCO, Mei Mwaka huu wa 2021.Alipata tuzo ya Super Woman
kipengele cha afya, tuzo ya 'Humanitarian of the Year', tuzo ya Malkia
wa nguvu 2017 na Tuzo ya Mwanamke wa mwaka 2020 iliyotolewa na Efm
kupitia kipindi cha Mwanamke cha Dina Marios.
Pamoja na tuzo hizo inatosha kuandika hapa kwamba mwaka 2014 Siku ya Wanawake Duniani taasisi ya MISA ilimtangaza kama moja ya wanawake mashuhuri wanaokuja kwa kasi na wa kuangaliwa. Na baada ya miaka saba Taifa la Tanzania linampa kazi ya kuiwakilisha katika balozi, kwenye kituo ambacho kina pilikapilika nyingi za mahusiano ya kimataifa cha Geneva, Uswizi baada ya mji wa New York, Marekani.
No comments:
Post a Comment