Anthony Ishengoma- Shinyanga.
Mkuu
wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati ameagiza TASAF Mkoa wa
Shinyanga kuhakikisha inawaweka wazee wote wasio kuwa na uwezo
wanaingizwa katika mpango wa kunusuru kaya masikini ili kupitia mpango
huo waweze kupata katika Bima ya Afya ya Afya iliyoboreshwa.
Aidha
Mkuu huyo wa Mkoa amesema bado kuna wazee ambao bado wanafanyiwa
vitendo vya ukatili ikiwemo kunyanyaswa na kubaguliwa ikiwemo mauaji na
kuendelea kuishi maisha magumu jambo ambalo linachangiwa na imani potofu
katika jamii hivyo kuwataka vijana kuwalinda wazee hao ili waweze
kuishi kwa amani kwani katika uzee binadamu anahitaji kupendwa.
Dkt.
Sengati amesema hayo leo wakati wa ufunguzi wa kikao cha robo mwaka cha
Baraza la wazee wa Mkoa wa Shinyanga na kuikumbusha jamii kutambua kuwa
kadili mwili wa binadamu unavyozeeka ndivyo viungo vinavyochoka hivyo
kufanya wazee kupata magonjwa nyemelezi kama vile kisukari, presha na
magonjwa mengine.
Dkt. Sengati aliongeza kuwa Mkoa wake una jumla
ya wazee 66,717 ambao kati yao wanaume ni 29,717 na wanawake 36,500 na
kati ya hao wazee wenye Bima ya Afya iliyoboreshwa 20,545 akiitaja idadi
hiyo kuwa ndogo sana ukilinganisha na idadi wazee iliyopo katika mkoa
wa Shinyanga na kutaka watendaji kuendelea kuimiza wazee kujiunga na
Bima ya Afya kwa ajili ya matibabu.
Naye Mzee Anderson Lymo
Katibu wa Wazee Mkoa wa Shinyanga amemuomba Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga
kuangalia zaidi suala matibabu ya wazee kwa kuwa suala la ukosefu wa
dawa kwa ajili ya matibabu ya wazee katika vituo vya Afya bado ni
changamoto kubwa kwa wazee hapa Nchini.
Mzee Lymo aliongeza kuwa
pamoja na upatikanaji wa Bima za Afya kwa wazee haitoshi kwani
changamoto iliyopo imekuwa ni upatikanaji wa madawa katika zahanati,
vituo vya Afya na hata hospitali kubwa na changamoto kubwa zaidi
inayowakumba wazee ni umasikini kwakuwa wengi hawana shughuli
inayowapatia kipato.
Wakati huo huo Mwenyekiti wa Braza la wazee
Mkoa wa Shinyanga Mzee Faustine Sengerema ameomba Mkuu wa Mkoa kuingilia
kati suala la wazee kushirikishwa katika ngazi mbalimbali za maamuzi
ikiwemo serikali za vijiji na maeneo mengine ili kuwawezesha wazee
kupaza sauti na kutoa ushauri kwa maendeleo ya Taifa.
Mzee
Sengerema alisema kuwa suala la wazee kushirika katika maamuzi
mbalimbali linatokana na miongozo mbalimbali iliyopo lakini utekelezaji
wake umekuwa haufanyiki hivyo kuwanyima wazee haki ya kushirikishwa
katika masuala mbalimbali ya mstakabali wa Nchi.
Baraza la Wazee
Mkoa wa Shinyanga linakaa kwa siku moja kufanya kikao chake cha robo
mwaka ikiwemo maandalizi ya uchaguzi wa Baraza jipya la wazee ambalo
lina wawakilishi kutoka Halmashauri zote sita zinazounda Mkoa wa
Shinyanga na mabaraza mengine kama hayo tayari yameundwa katika mikoa
mbalimbali hapa Nchini.
Mwenyekiti
wa Baraza la wazee Mkoa wa Shinyanga Mzee Faustine Sengerema akiongea
na baadhi ya Wazee hawapo pichani walioshiriki kikao cha Baraza hilo leo
Mkoani Shinyanga.
Baadhi
ya Wazee walioshiriki kikao cha Baraza la Wazee cha Mkoa wa Shinyanga
wakisoma dua kabla ya kuanza kikao chao leo leo Mkoani Shinyanga.
Viongozi wa Baraza la Wazee Mkoa wa Shinyanga wakishiriki sala kabla ya kuanza kikao chao leo Mkoani Shinyanga.
No comments:
Post a Comment